JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Chadema ‘Kimewaka’

Chimbuko migogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unasababishwa migongano wa kupata madaraka ndani ya chama hicho, JAMHURI limebaini

Imelezwa kuwa mtafaruku uliotokea mwishoni mwa wiki na kusababisha kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa  Mkoa wa Arusha wa Chadema  kwa muda usiojulikana ni mgongano wa kutafuta madaraka ndani ya chama hicho.

‘Majangili’ 20 hatari

  • JWTZ watisha, maofisa Maliasili 16 wakamatwa
  • Mmoja akutwa anamiliki bunduki 5 za rifle kali
  • Mbunge Mtutura ahojiwa, Nchambi naye atajwa
  • RCO aliahidiwa dola 3,000 akawaachia Waarabu

Operesheni Tokomeza inayoendeshwa chini ya usimamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), imewakamata watumishi kadhaa wa Serikali wanaotuhumiwa kujihusisha na ujangili. Operesheni hiyo inaongozwa na Luteni Kanali A. Sibuti.

Rushwa yazigonganisha Mahakama, Wizara

Wizara ya Nishati na Madini imeingia kwenye mvutano na Mahakama baada ya mhimili huo kuamuru raia wa China aliyekamatwa akitorosha madini ya tanzanite, arejeshewe madini hayo kinyume cha sheria.

Maswi: Kila Mtanzania atapata umeme

Serikali kupitia Wizara ya Nishati na Madini imesema umeme ni huduma ya lazima kwa Watanzania na itafanya kila liwalo kuhakikisha kila Mtanzania anapata umeme. Msimamo wa Serikali umetolewa na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wakati akizungumza katika kipindi cha Tuambie kupitia runinga ya Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), wiki iliyopita.

DECI mpya yaibuka Dar

Kituo cha Mafunzo ya Ujasiriamali Tanzania kilichopo jijini Dar es Salaam, kimeingia katika kashfa ya kuwatapeli wajasiriamali walioshiriki katika semina  za ufugaji kwa kuwapa ahadi hewa.

JWTZ yafyeka majangili

*Operesheni Tokomeza’ yaanza rasmi

*Inashirikisha, Usalama wa Taifa, Polisi

*Majangili kadhaa hatari yakamatwa

 

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeanza rasmi operesheni ya kuwatokomeza majangili.

Operesheni hiyo iliyopewa jina la Operesheni Tokomeza ilianza rasmi Oktoba 5, mwaka huu ikilenga kuwalinda wanyamapori, hasa ndovu na faru walio hatarini kumalizwa na majangili.