JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Bosi NIC ang’olewa

* Bodi yakatisha mkataba ghafla

* Afika ofisini akuta kufuli mlangoni

* Mwenyewe adai umri wa kustaafu

Mkurugenzi wa Shirika la Bima la Taifa (NIC), Justine Peter Mwandu, sasa ameondolewa kazini akiwa amebakiza mkataba wa zaidi ya mwaka mmoja wa utumishi wake, imefahamika jijini Dar es Salaam.

Mwekezaji ahusishwa kifo Katibu wa Chadema

Watu watatu akiwamo Polisi Jamii wa Kijiji cha Ming’enyi, Kata ya Gehandu, Hanang mkoani Manyara, wanadaiwa kumuua Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tawi la Kijiji, Andu Kero.

Lissu amuonya Chenge

*Asema mchezo wa kutumia mahakama haumsaidii

*Amdonoa Rais JK, awatahadarisha wasaidizi wake

*Ataka Jaji Werema afikishwe mahakamani haraka

*CCM yawatosa rasmi Chenge, Prof. Tibaijuka, Ngeleja

 

 

Mwanasheria Mkuu wa chama kikuu cha upinza – Chama cha Maendeleo na Demokrasi (CHADEMA), Tundu Lissu amesema Mwanasheria Mkuu wa zamani wa Serikali, Andrew Chenge anachokifanya mbele ya macho ya Watanzania kwa sasa ni kukwepa kujieleza hadharani.

Mjane Geita aelezea Finca ilivyompora mali

Yakomba majokofu mawili, televisheni, deki

Pia jenereta kubwa kwa deni la Sh. 600,000

Mama aona maisha magumu, ataka kujiua

 

Malalamiko dhidi ya Benki ya FINCA Tanzania, Tawi la Geita, kwamba inanyanyasa wajasiriamali, yamemuibua mjane aliyeeleza alivyoporwa kwa mabavu vitu vyake vyenye thamani ya zaidi ya Sh milioni 1.65 kabla ya kuuzwa kwa bei ya Sh 600,000.

Waziri afagilia ‘JAMHURI’ wa akisimamia bomoabomoa

Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, George Simbachawene, Alhamisi iliyopita alishindwa kuzuia hisia zake, pale alipolipa sifa Gazeti la JAMHURI huku akisimamia ubomoaji wa mgahawa uliojengwa katika eneo la wazi jijini.

Sadifa atangaza vita dhidi ya Maalim Seif

 

.Amtuhumu kuwa ni kibaraka wa Waarabu

.Adai Seif akipewa nchi, ataiuza asubuhi

.Rais Dk. Shein amsifu Sadifa hadharani

.CUF waijia juu Polisi, wadai Sadifa ni…

 

 

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), Khamis Sadifa Juma, ametangaza hadharani vita ya kupambana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad.