Category: Kitaifa
Madiwani Chadema Geita wafichua ufisadi wa bil 11/-
*Tamisemi, Hazina, CCM wahusishwa
Madiwani watatu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wa Halmashauri ya Mji wa Geita, kwa kushirikiana na mmoja wa Viti Maalum wa Halmshauri ya Wilaya ya Geita, wametoa nyaraka katika mkutano hadhara uliofanyika Julai 14, mwaka huu, zinazoonesha wilaya hiyo kupokea Sh bilioni 11 kwa ajili ya ununuzi wa madawati lakini matumizi yake hayajulikani.
Wasira: Nivigumu kuifuta Chadema
*Akiri kuwa kazi hiyo si nyepesi
Kukifuta Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) si rahisi; amethibitisha Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uhusiano na Uratibu), Stephen Wasira.
Wanaume watelekeza watoto walemavu Arumeru
*Wanawake wasukumiwa mzigo
Tatizo la wanaume kuwatelekeza watoto wao wenye ulemavu, limetajwa kukithiri katika Kijiji cha Ambureni, Wilaya ya Arumeru, mkoani Arusha.
Ulaji ugeni wa marais 11
Kampuni ‘hewa’ zakomba mamilioni
*CAG atakiwa aingie kazini mara moja
Kampuni tatu kati ya nane zilizozawadiwa zabuni tata za vifaa na huduma kwenye Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), zimebainika kuwa ni ‘hewa’.
Waziri Mku: Tutavuna gesi asilia baada ya miaka kumi
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amesema mavuno ya gesi asilia iliyopo mkoani Mtwara yataanza kupatikana baada ya kipindi kisichopungua miaka kumu.
Nchi imetafunwa!
*Hazina yatumia Shilingi bilioni 8, taasisi za umma
zachangishwa, ‘wajanja’ watafuna mamilioni
*Vifaa vya Obama vyaokoa jahazi, sare, mikoba, vyagharimu
mil. 400/-, vinyago navyo balaa!
*Karamu, chupa za kahawa, miavuli mil. 390/-,
Burudani ya muziki yatafuna milioni 195/-
*Dewji agoma kuchangia, Katibu Mkuu Haule
arushiwa kombora, yeye ajitetea
Mkutano wa Majadiliano ya Kimataifa ya Ushirikiano kwa Manufaa ya Wote (Smart Partnership Dialogue), uliomalizika hivi karibuni jijini Dar es Salaam, umeigharimu Serikali Sh bilioni nane.