Category: Siasa
Matusi kwa Rais wetu hayakubaliki
Kwa muda sasa, kumekuwapo maneno mengi kutoka kwa Rais Paul Kagame wa Rwanda yakimlenga Rais wetu, Jakaya Kikwete. Chanzo cha yote haya ni mapendekezo ya Rais Kikwete ya kumwomba Rais Kagame aketi na waasi wa kundi la FNBL ili kukomesha mapigano na mauaji yanayoendelea Rwanda na upande wa mashariki kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
Iddi Simba lazima ashitakiwe upya
Ugeni mkubwa uliofika hapa nchini umeshaondoka. Ugeni huo ni wa Rais Barack Obama wa Marekani, Rais mstafu George W. Bush wa Marekani, marais zaidi ya 10 kutoka mataifa mbalimbali Afrika na duniani kwa jumla, pamoja na mawaziri waandamizi kutoka mataifa mbalimbali.
Tuwe makini ugawaji mikoa, wilaya
Rais Jakaya Kikwete ametoa baraka za ugawaji Mkoa wa Mbeya ili ipatikane mikoa miwili.
Tayari ameshafanikisha uanzishaji mikoa minne ya Simiyu, Njombe, Katavi na Geita. Pamoja na mikoa hiyo, ameanzisha wilaya nyingi mpya.
vVyombo vya dola visimchekee polisi huyu
Wiki iliyopita, Jeshi la Polisi lilimtia mbaroni mmoja wa askari wake, baada ya kumkuta akiwa na risasi 200 ambazo haijajulikana alikotaka kuzipeleka.
Bravo CHADEMA, CUF mmeonesha ukomavu
Wiki iliyopita, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Chama cha Wananchi (CUF) vilionesha ukomavu wa kisiasa.
Wachochezi wa vurugu waadabishwe ipasavyo
Wiki iliyopita, Jeshi la Polisi lilitangaza kumtia mbaroni mtu anayedaiwa kuwa kinara wa kusambaza ujumbe wa kuchochea chuki na uhasama hapa nchini, kupitia simu za kiganjani.