Category: Siasa
JAMHURI YA WAUNGWANA
Kwa mwaka Mtanzania hafanyi kazi kwa siku 140!
Makala yangu ya wiki iliyopita ya “Wakati mwingine Wakristo wanaanzisha chokochoko”, imepokewa kwa hisia tofauti na wasomaji wa safu hii.
Makala ililenga kupinga msimamo wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) wa kutaka Jumapili isitumike kwa kura ya maoni inayotarajiwa kupigwa kama sehemu ya kupata Katiba mpya.
Mapambano dhidi ya wauza ‘unga’ ni mzaha mtupu
Nazungumzia Serikali inayoendesha mapambano dhidi ya dawa za kulevya. Nionavyo mimi ni mzaha mtupu. Ni sawa na kukumbuka kujifunika shuka wakati kumeshakucha.
Kabantega: Mzalendo anayekabiliwa na kifo kama Dk. Masau
*Ni bingwa wa kutengeneza test tube aliyetelekezwa
*Miaka 27 sasa anapigwa danadana na wakubwa serikalini
*Mitambo, malighafi alivyozawadiwa vinaozea bandarini
*Mwalimu Nyerere, Rais Kikwete, Lowassa walimkubali
*Umoja wa Mataifa, AU, Sudan Kusini, Rwanda wanamlilia
Mwaka 2009 nilikutana na Mtanzania aliyenivutia kwa ubunifu, uwezo wake wa kiakili, na zaidi ya yote ni uzalendo wake kwa nchi yake. Nikamwomba na yeye akakubali kufanya mahojiano. Lengo lilikuwa kuwawezesha Watanzania, hasa watu wenye mamlaka ya uongozi waweze kumtambua, kumsaidia na kumtumia ili ndoto yake itimie.
BARUA ZA WASOMAJi
Barua ya wazi kwa Waziri wa Maji
Mheshimiwa Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe, hongera kwa kazi, siwezi kukupa pole kwani kazi ni wajibu na kipimo cha mtu.
Ansar Sunni: Hatumtambui Sheikh Ponda
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu wa Ansar Sunni, Sheikh Salim Abdulrahim Barahiyan, amesema jumuiya hiyo haina uhusiano na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Waislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda. “Mimi sijawahi kukaa na Sheikh Ponda katika kikao hata kimoja. Tuna misikiti karibu 20 Tanga, hajawahi kuingia hata msikiti mmoja,” amesema Sheikh Barahiyan.
Barua ya wazi kwa Waziri Mwakyembe
Mheshimiwa Waziri Dk. Harrison Mwakyembe, tunayo heshima kuchukua nafasi hii kukujulisha kuwa matrekta haya unayoyaona yamekwishalima sana na sasa hayawezi kazi hiyo tena. Ukiyafukuza mjini ni wazi hayatakwenda kulima, maana mengi hayana uwezo tena wa kufanya kazi hiyo.