Category: Makala
MISITU & MAZINGIRA
Misitu inavyoinufaisha Nanjilinji ‘A’ (4)
Pongezi kwa wananchi wa Nanjilinji ‘A’
Kwa kuzingatia mafanikio yaliyopatikana katika Kijiji cha Nanjilinji ‘A’ na kwa kuelewa kuwa mafanikio hayo yametokana na wanakijiji kudhamiria kwa dhati kutumia rasilimali misitu inayopatikana ndani ya mipaka ya kijiji chao bila kushurutishwa na mtu yeyote, napenda nichukue fursa hii kutoa pongezi zangu za dhati kwa uongozi wa kijiji na wakazi wake wote kwa mafanikio hayo ya kutia moyo.
KONA YA AFYA
Vidonda vya tumbo na hatari zake (10)
Wiki iliyopita, Dk. Khamis Zephania alielezea dalili za vidonda vya tumbo yakiwamo maumivu na tofauti yake kulingana na rika. Sasa endelea kumfuatilia katika sehemu hii ya kumi…
Tony: Nauza kahawa na digrii yangu
*Ni mhitimu wa Chuo Kikuu Dar es Salaam
*Anauza kahawa stendi ya mabasi Ubungo
*Awaasa wasomi kutodharau kazi, aeleza mazito
Wakati vijana wengi waliohitimu elimu ya chuo kikuu wakikumbatia dhana ya kutarajia kuajiriwa serikalini na kwenye kampuni kubwa, hali ni tofauti kwa Tony Alfred Kirita, mhitimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).
KAULI ZA WASOMAJI
Askari GGM wanatumaliza
Viongozi wa Wilaya ya Geita wajue kuwa askari maarufu kama ambush na wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) katika Mgodi wa Dhahabu wa Geita (GGM) wanatutesa sana, baadhi yetu wanafanywa vilema na wengine wanauawa. Wapo watu wengi wamekufa kutokana na kupigwa risasi. JAMHURI tusaidieni kupigia kelele tatizo hili, tunakwisha!
Paulo, Geita
0758 479 354
Watanzania tukazane kuwekeza kwenye ardhi
Leo ni mwaka mmoja kamili umepita tangu nilipoandika makala hapa safuni yaliyokuwa na kichwa, “Njooni shambani mtajirike”. Ilikuwa ni makala yaliyotoa shime kwa Watanzania kuchangamkia fursa ya uwekezaji kwenye kilimo cha miti.
NUKUU ZA WIKI
Julius Nyerere: Kumteta mtu ni kumdhuru
“Wengine humwona mwenzao anafanya kosa, badala ya kumwambia pale pale kijamaa kwamba atendalo ni kosa, watanyamaza kimya. Lakini hawanyamazi kabisa! Watakwenda kumteta katika vikundi vya siri siri. Mateto haya si ya kumsaidia mwenzao, ni ya kumdhuru.”
Maneno haya ni ya Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Ndiye Rais wa Kwanza wa Tanganyika na baadaye Tanzania.