JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

FIKRA YA HEKIMA

LAAC imechelewa kugundua
madudu hazina, halmashauri

Ijumaa iliyopita, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC), ilitangaza kugundua mtandao wa wizi wa mabilioni ya shilingi za umma. Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Rajab Mohamed Mbarouk, alisema mtandao huo unahusisha ofisi za Hazina na halmashauri mbalimbali hapa nchini.

TBS yadhibiti uharibifu injini za magari

Kuzinduliwa kwa mtambo mpya wa kupima mafuta kunaashiria kwisha kwa tatizo la muda mrefu la kuharibika kwa injini za magari yanayotumia mafuta ya petroli nchini. Mtambo huo wa kisasa uliozindulia wiki iliyopita na Waziri wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda,  jijini Dar es Salaam, ni miongoni mwa mitambo inayopima mafuta ya magari iliyopo katika maabara ya kemia.

BARUA ZA WASOMAJi

Bukoba kulikoni?

Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Meya, Balozi Kagasheki tuambieni kulikoni Bukoba? Tuambieni wakweli ni wapi kati ya madiwani waliofukuzwa, meya na madiwani waliobaki. Tuambieni tatizo ni nini hasa? Kimefichika nini hasa?

FASIHI FASAHA

Tusizikwe tungali hai – 2

Katika sehemu ya kwanza niligusia watangazaji wastaafu na chama chao VEMA, dira na malengo ya sera ya habari na utangazaji, na watangazaji wa ‘dot com’ na vyombo vya utangazaji. Dhana hizo tatu zimo katika mgongano wa mawazo kuhusu kuhabarisha, kuelimisha na kuburudisha Watanzania.

Yah: Tunashindwaje kukabili vifo vya kujitakia?

Nataka niwe mtu wa tatu kupigana na utaratibu wa maisha ya Mtanzania kuwekewa mazingira ya kifo ambayo hakustahili, mazingira haya yanatayarishwa bila mtayarishaji na anayetayarishiwa kujua kuwa anaandaliwa mazingira ya kifo.

KONA YA AFYA

Vidonda vya tumbo na hatari zake (9)

Katika sehemu ya nane ya makala haya, Dk. Khamis Zephania alizungumzia pamoja na mambo mengine, madhara ya kazi za usiku, makundi ya damu na uhusiano wa vidonda vya tumbo. Sasa endelea na sehemu hii ya tisa…