JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Tujenge misingi ya umoja ili tuelewane

Nataka kusisitiza nini: Kwamba sisi ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere aliyealikwa kuwa mgeni rasmi kwenye kilele cha Sikukuu ya Wafanyakazi Duniani iliyofanyika kitaifa Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya Mei Mosi, 1995. Katika hotuba yake, Mwalimu alielezea historia ya vyama vya wafanyakazi duniani. Aidha, alitumia fursa hiyo kutoa maoni yake kuhusu hali ya kisiasa na kiuchumi nchini pamoja na ushauri kuhusu mambo ambayo wananchi wanapaswa kuzingatia wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba mwaka huo, hasa sifa za wagombea nafasi za uongozi kuwa ni pamoja na kila mmoja kujiuliza ataifanyia nini nchi yake baada ya kuchaguliwa na anakwenda kufanya nini Ikulu. Ifuatayo ni hotuba ya Mwalimu.

Mwigulu kata pua uunge wajihi

Juma lililopita nikiwa nafuatilia Kikao cha Pili cha Mkutano wa Bunge, nilimshuhudia na kumsikia Mbunge wa Iramba Magharibi, Mwigulu Nchemba, akieleza matukio ya vifo vya raia katika maeneo kadhaa nchini, vilivyotokea kwenye shughuli za kisiasa na akahoji nafasi ya kisheria kuwashughulikia wahusika na waratibu wa matukio hayo badala ya wale wanaoshiriki katika maelezo yake.

Matakwa ya Rwanda yasiivunje EAC

 

Kwa muda wa mwezi mmoja sasa uhusiano baina ya Tanzania na Rwanda umezorota. Uhusiano huo umezorota baada ya matukio mawili. Tukio la kwanza ni ushauri  Rais Jakaya Kikwete aliompa Rais Paul Kagame wa kuzungumza na waasi wa kundi la FDLR kwa nia ya kurejesha amani. La pili ni Tanzania kupeleka majeshi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kupambana na waasi wa M23.

Hii ndiyo dawa ya kuepuka bomoabomoa

Katika miaka ya 1980, bendi moja ya muziki wa dansi hapa nchini ilitunga wimbo uliokuwa na kibwagizo cha “bomoa ee, bomoa ee, tutajenga kesho!”

Misitu inavyoinufaisha Nanjilinji ‘A’ (5)

Katika sehemu ya nne, Dk. Felician Kilahama alizungumzia kazi ya kutoa huduma bora za kijamii na kujenga miundombinu imara katika nchi yenye eneo kubwa. Alisema shughuli hiyo inahitaji ujasiri mkubwa na uzalendo wa hali ya juu. Sehemu hii ya tano na ya mwisho, Dk. Kilahama anatoa hitimisho.

MISITU & MAZINGIRA

Misitu inavyoinufaisha Nanjilinji ‘A’ (4)

Pongezi kwa wananchi wa Nanjilinji ‘A’

Kwa kuzingatia mafanikio yaliyopatikana katika Kijiji cha Nanjilinji ‘A’ na kwa kuelewa kuwa mafanikio hayo yametokana na wanakijiji kudhamiria kwa dhati kutumia rasilimali misitu inayopatikana ndani ya mipaka ya kijiji chao bila kushurutishwa na mtu yeyote, napenda nichukue fursa hii kutoa pongezi zangu za dhati kwa uongozi wa kijiji na wakazi wake wote kwa mafanikio hayo ya kutia moyo.