Category: Makala
Taifa linawahitaji ‘wajasiriakazi’
Nimekuwa nikiandika makala za hamasa kuhusu ujasiriamali, ikiwa ni hatua ya kukabiliana na mabadiliko ya kiuchumi ambapo kuna upungufu mkubwa wa ajira, lakini pia kuna mfumko wa gharama za maisha kiasi kwamba hata walioajiriwa wanapata wakati mgumu kumudu vema maisha ya kila siku.
Siasa inavuruga masuala ya Taifa
Tunapozungumzia siasa hatuwezi kudai kwa haki kwamba siasa ni kitu kibaya. Ungeweza kusema kwamba siasa ni maneno mazuri yanayomtoa nyoka pangoni. Kwa kifupi siasa inasaidia kutatua matatizo.
Benki ya NMB yaanzisha mikopo ya bajaj
Benki ya NMB imeanza kutoa mikopo ya pikipiki zinazotumia magurudumu matatu (bajaj) kwa wajasiriamali nchini.
Tuache kufyatua maneno – 2
Katika Kamusi hiyo, neno, ‘ari’ linaainishwa kuwa ni “hamu ya kutaka kukamilisha jambo na kutokubali kushindwa; ghaidhi, hima, nia, kusudio’. Hii ina maana kwamba matumizi ya neno ‘changamoto’ yameachanishwa na ufafanuzi wa Kiswahili.
Jukwaa la Wakristo limenishangaza
Jukwaa la Wakristo Tanzania (TCF) linalojumuisha Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT), Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekosti Tanzania (PCT) na Kanisa la Waadventisti Wasabato (SDA), limenishangaza. Limenishangaza kwa lililolitoa hivi, kufuatia mkutano wake wa dharura uliofanyika Kurasini, Dar es Salaam, Machi 8 mwaka huu, ukiwahusisha maaskofu 117 wa makanisa mbalimbali nchini.
Kamati ya Pinda imalize mgogoro wa uchinjaji
Mwanzoni mwa mwaka huu, uliibuka uhasama mkubwa uliohusisha pande mbili za dini ya Kiislamu na Kikristo mkoani hapa. Uhasama huu ulianza kama ‘mchicha’ kwa viongozi wa pande hizi mbili kuzuliana visa kutokana na nani au dini gani inastahili kupewa heshima ya kuchinja wanyama kwa ajili ya kitoweo.