Operesheni za al-Shabaab zadhoofishwa Kenya

Operesheni za usalama zinazofanywa kwa msaada na jamii zimedhoofisha uwezo wa kundi la wanamgambo la al-Shabaab kufanya mashumbulizi nchini Kenya. Tangu Februari 17, wakati wanachama wa al-Shabaab waliposhambulia kituo cha polisi katika eneo la Jarajila mjini Garissa, na kumuua polisi mmoja, hapajatokea mashambulizi yoyote yanayohusishwa moja kwa moja na al-Shabaab katika eneo hili, Kamishna wa Jimbo la Kaskazini Mashariki, James ole Seriani, alisema mwishoni mwa wiki.

Read More