JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Makala

Serikali ni mtuhumiwa pekee kipigo cha Dk. Ulimboka

Mkononi nina Gazeti la JAMHURI (Julai 10-16, 2012) toleo Na. 33. Nimevutiwa na kichwa cha habari, ‘Dk. Ulimboka siri zavuja’. Nimevutiwa na habari hii kwa sababu ni moja ya mambo yanayoigusa jamii kwa sasa ikizingatiwa kuwa bado hali yake kwa walio wengi hatuijui, lakini pia mgomo wa madaktari bado unaendelea (naomba mgomo huo uishe ili tuweze kupata huduma).

Siri ya mafanikio yangu kiuchumi

Sasa nimeamini kuwa ‘la kuteleza haliwezi kutembea’ na ‘la kuvunda halina ubani’. Wiki mbili zilizopita niliandika makala yaliyokuwa na kichwa chahabari, ‘Je, machozi ya walimu yatamimina fedha mitaani?’

Mchechu: Tanzania si masikini

“Maelezo kwamba Tanzania ni nchi masikini yananikera. Imefika mahala wanasiasa wanadhani ili uwe kiongozi bora ni lazima ujiainishe kuwa unatatea masikini. Natamani tukose misaada kwa miaka mitano, tutapata akili na kutumia vyema utajiri tulionao. Hatustahili misaada kabisa maana nchi hii inao utajiri wa kutosha.”

Maneno haya ameyasema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu, akiwaambia wahariri wa vyombo vya habari mjini Morogoro kuwa mawazo ya Watanzania yanapaswa kufikiria kufanya kazi zaidi badala ya kutegeshea misaada.

‘Uhai wa raia unaangamia kwa kukosa ulinzi wa tiba’

UJUMBE WA BARAZA LA MAASKOFU KATOLIKI TANZANIA KWA WAUMINI WAKATOLIKI NA WATU WOTE WENYE MAPENZI MEMA

 

Sisi Maaskofu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania tumekutana katika Mkutano wetu Mkuu wa 65 wa kawaida tangu tarehe 23-30 Juni 2012 uliowajumuisha Wakuu wa Mashirika ya Kitawa, wakuu wa Idara, Tume na Taasisi za Baraza pamoja na wawakilishi Walei.

 

Gandhi: Woga ni hatari

“Hakuna jambo baya linalomharibu binadamu kama woga, na yeyote anayemwamini Mungu anapaswa kujisikia aibu kwa kupata woga juu ya chochote [katika dunia hii].”

Haya ni maneno ya mpigania Uhuru wa India, Mahatma Gandhi aliyoyatoa wakati akiwahamasisha Wahindi kujenga mshikamano.

***

Tuwafundishe wasomi wetu kujiajiri

 

Miezi ya karibuni kule nchini Marekani askari walipambana na waandamanaji waliokuwa wakilalamika kuongezeka kwa pengo kati ya wenye nacho na wasio nacho.

 

Mara kadhaa waandamanaji hao wamejaribu kuandamana kupitia njia mbalimbali, ikiwamo ile ya kukutana kwenye daraja la Mto Mississipi lakini mara zote wameambulia kufurumushwa na polisi.