Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akifanya mazungumzo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Ikulu, Zanzibar leo tarehe 22 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiagana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ikulu, Zanzibar leo tarehe 22 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akisalimiana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, wakati alipowasili Ikulu, Zanzibar leo tarehe 22 Novemba 2025.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi akiwa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, katika picha ya pamoja na Viongozi mbalimbali, mara baada ya mazungumzo yaliyofanyika Ikulu, Zanzibar leo tarehe 22 Novemba 2025. (kutoka kulia ni Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Zanzibar Salehe Juma Mussa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Zanzibar Dkt. Saada Mkuya, Katibu wa Baraza la Mapinduzi na Katibu Mkuu Kiongozi, Zanzibar Mhandisi Zena Said, Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhandisi Cyprian Luhemeja na Katibu wa Makamu wa Rais Bw. Edwin Makamba) 

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amempongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kwa ushindi wa kishindo aliyoupata katika Uchaguzi Mkuu, Oktoba 2025.

Makamu wa Rais ametoa pongezi hizo wakati akizungumza na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Zanzibar. Amesema ushindi huo ni matokeo ya kazi kubwa aliyofanya Dkt. Mwinyi pamoja na Chama Cha Mapinduzi katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.

Kwa upande wake Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amempongeza Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi, kwa kushika wadhifa huo, na kumuhakikishia kuendelea kufanya kazi kwa karibu na Ofisi ya Makamu wa Rais katika kutafuta ufumbuzi wa masuala mbalimbali ya kimuungano.

Makamu wa Rais Dkt. Nchimbi, amefika Ikulu Zanzibar kwa lengo la kujitambulisha.