Na Mwandishi Wetu, JamhuriMedia, Katavi

Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Katavi, Mhandisi Andrew Mwalugaja, ameendelea kuwa mstari wa mbele katika kuongoza sekta ya madini kwa uwajibikaji, weledi na ubunifu. 

‎Kupitia usimamizi wake, Katavi imepiga hatua kubwa katika kuboresha mazingira ya uwekezaji, kuongeza kasi ya utoaji wa leseni, kuimarisha usalama na kufungua masoko mapya ya madini.

‎Uongozi wake umeimarisha ushirikiano kati ya Serikali, wawekezaji na wachimbaji, hatua iliyobadilisha taswira ya Katavi na kuufanya mkoa huo kuwa kitovu kipya kinachoongoza kwa fursa za uwekezaji wa madini nchini.