Israel imesema kwamba imefanya mashambulizi ya anga kwenye mji wa bandari wa Hodeida wa Yemen na maeneo mengine yanayoshikiliwa na waasi wa Huthi.
Israel imesema kwamba imefanya mashambulizi ya anga kwenye mji wa bandari wa Hodeida wa Yemen na maeneo mengine yanayoshikiliwa na waasi wa Huthi.
Katika taarifa hiyo leo, Israel imesema ndege zake za kivita “zimeshambulia na kuharibu miundombinu iliyo chini ya utawala wa waasi wa Kihuthi na miongoni mwa maeneo waliyoyalengwa yakiwa ni bandari za Hodeida, Ras Isa na Salif”.
Israel imesema mashambulizi hayo ni “majibu ya mashambulizi ya mara kwa mara ya Wahuthi dhidi ya taifa la Israel”.
Waasi wa Huthi wa Yemen ambao wanawaunga Wapalestina wamekuwa wakirusha makombora na droni huko Israel tangu vita vya Gaza vilipozuka Oktoba 2023 baada ya kundi la wanamgambo wa Palestina wa Hamas kushambulia Israel.
