Wafuasi wa Raila Odinga wamevamia lango kuu la uwanja wa ndege wa JKIA baada ya kuwazidi nguvu polisi waliokuwa wakilinda eneo hilo.

Hali ya taharuki imetanda, huku kukiwa na wasiwasi mkubwa juu ya kitakachotokea endapo watapenya na kuingia ndani ya uwanja huo.

Serikali imeongeza kikosi cha jeshi kwa dharura ili kudhibiti hali kabla haijazidi kuwa mbaya.