Marekani inataka makubaliano kati ya Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kujumuisha Rwanda kuyaondoa majeshi yake kutoka Mashariki mwa Congo kabla pande hizo mbili kutia saini makubaliano ya amani.

Duru zinaarifu kuwa rasimu ya makubaliano ya amani inaanisha kuwa sharti Rwanda iyaondoe majeshi yake,silaha na vifaa vyake mashariki mwa Congo ndipo makubaliano hayo yatiwe saini.

Utawala wa Rais wa Marekani Donald Trump umekuwa ukisimamia mazungumzo ya kuvimaliza vita vya Congo na kuhakikisha uwekezaji hasa katika sekta ya madini

Mshauri mkuu wa Trump kuhusu Afrika Massad Boulos mnamo mwezi uliopita,alisema anataka makubaliano ya amani kuafikiwa katika kipindi cha miezi miwili,muda ambao wachambuzi wanautilia mashaka ikizingatiwa matatizo yaliyokita mizizi yanayochochea uhasama kati ya DRC na Rwanda.

Serikali ya Rais Felix Tshisekedi imekuwa ikiishutumu vikali Rwanda kuunga mkono kundi la waasi la M23,madai ambayo Rwanda mara kwa mara imekuwa ikiyakanusha. Rwanda imekuwa ikisema kuwa inalinda mipaka yake na Congo kutokana yapo Congo na tisho dhidi ya waasi wa Kihutu (FDLR)wanaoutuhimiwa katika mauaji ya halaiki ya mwaka 19994 yaliyowaua karibu watu milioni moja, wanaohatarisha usalama wake. Imeilaumu pia serikali ya Kinshasa kwa kuwaingiza wanamgambo hao katika jeshi lake.

Duru zinasema Rwanda bado haijatoa msimamo wake kuhusu rasimu hiyo ya makubaliano. Waziri wa mambo ya nje wa Rwanda Olivier Nduhungirehe ameliambia shirika la Reuters kuwa wataalamu kutoka Congo na nchi yake watakutana wiki hii mjini Washington kujadili zaidi makubaliano hayo.

Hata hivyo Congo inahisi Rwanda inajikokota katika kufikia makubaliano ya amani ikisisitiza kuwa ili mchakato huo wa amani ufanikiwe,Rwanda lazima iondoe majeshi yake na ikome kuwaunga mkono waasi wa M23.

Serikali ya Congo pia inafanya mazungumzo mengine na waasi hao yakisimamiwa na Qatar lakini walio na ufahamu na yanayojiri katika mazungumzo hayo ya Doha wanasema hakuna juhudi kubwa zilizopigwa na pande zote mbili.