JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Tanzania na biashara za kishirikina

Wiki iliyopita niliandika makala yaliyokuwa na kichwa, “Je kufanya biashara ni kipaji?” Ninafurahi kuwa yamekuwa makala yaliyowavutia wengi ambao hawakusita kunitumia mirejesho ya pongezi na maoni kupitia ujumbe wa simu, barua pepe na simu za miito. Msomaji mmoja amenitumia ujumbe ulionifurahisha kweli kweli; ninanukuu, “Makala yako ni nzuri na umechambua kitaalamu, lakini pia utajiri wa Wakinga asilimia 70 huwezi kuutenganisha na ushirikina. Vile vile Wachagga nao utajiri wao asilimia 30 ni ushirikina na 20% ni ujambazi. Na asilimia zilizobaki ndizo zinazoangukia kwenye uchambuzi wako,”  mwisho wa kunukuu. Leo nitachambua kwa mara nyingine tena hili sekeseke la ushirikina kuhusishwa na biashara, si tu kwa Wakinga na Wachagga pekee, bali pia kwa wafanyabiashara wote bila kujali kabila wala eneo waliloko. Lakini kabla ya kuendelea na uchambuzi huu kwanza nina taarifa moja ya muhimu kwa wasomaji wetu.

Golikipa mwanamke ashinda tuzo Ujerumani

Golikipa wa Timu ya Taifa ya Wanawake ya Ujerumani, Nadine Angerer, ameshinda tuzo ya mwanamke bora mcheza soka barani Ulaya.

Vitisho vya Mahakama kwa gazeti Jamhuri

Septemba 3, mwaka huu, Jaji Kiongozi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Fakihi Jundu, aliitisha mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam na kutoa taarifa ifuatayo:

TAARIFA YA MAHAKAMA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU HABARI ILIYOANDIKWA NA GAZETI LA JAMHURI; LIKIWATUHUMU WAH; MAJAJI NA MAHAKIMU KUWALINDA WAFANYABIASHARA WA  DAWA ZA KULEVYA

Hivi karibuni imekuwa ni kawaida kusikia Majaji, Mahakimu au kesi mbalimbali zilizo mahakamani zikiendelea kusikilizwa, au maamuzi fulani yaliyotolewa na mahakama kulalamikiwa katika vyombo vya habari, na hatimaye watoe maamuzi husika au wasikilizaji wa kesi husika, ambazo nyingine huwa bado zinaendelea mahakamani kudhalilika na kuhukumika, na wakati mwingine, ushahidi kuharibika au kumshawishi Jaji au hakimu kutoa maamuzi kwa kufuata maoni ya magazeti, na ilhali maadili ya kazi za ujaji hayatoi mamlaka kwa walalamikiwa kujibu kwa kukanusha shutuma zilizo mbele yao kwa njia ya vyombo vya habari.

NUKUU ZA WIKI

Julius Nyerere: Nchi haiendelei bila viwanda vya kisasa

“Maana ya maendeleo ya leo ya uchumi wenye nguvu ni maendeleo ya viwanda. Nchi yenye viwanda tunasema ni nchi iliyoendelea. Hata hivyo, tuna maana nyingine ya nchi zilizoendelea ya kuziita ni nchi zenye viwanda. Nchi haiwezi kuendelea bila kuwa na viwanda vya kisasa.

FIKRA YA HEKIMA

Kampuni za simu za mkononi  zinaiba umeme, hatutapona

Wakati Wizara ya Nishati na Madini ikiwaaga vijana 10 wazawa wanaokwenda China kusomea shahada ya uzamili kuhusu fani ya mafuta na gesi wiki iliyopita, Shirika la Taifa la Umeme Tanzania (TANESCO) limetangaza kubaini wizi wa nishati ya umeme kwenye minara ya kampuni za simu za kiganjani.

Pinda apotoshwa, Takukuru yapigwa chenga Geita

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipewa taarifa zinazoaminika kuwa alidanganywa na Afisa Kilimo wa Wilaya ya Geita, kuhusu utekelezaji wa mradi wa umwagiliaji katika vijiji viwili vya Nyamboge na Nzela wilayani hapa.