Latest Posts
Malaika kuingia sokoni kwa staili tofauti
Uongozi wa Bendi mpya ya muziki wa dansi ya Malaika iliyoundwa hivi karibuni, umesema kuwa umeamua kufanya muziki kwa kuzingatia ubunifu, tofauti na zilivyo bendi nyingine za muziki huo ili kukamata soko.
Katiba haiandikiki
- CCM, Chadema, Profesa Shivji wasema muda hautoshi
- Jaji Mtungi aonya, mnyukano waendelea, hofu yatanda
Kuna kila dalili kuwa Katiba mpya iliyotarajiwa kuzinduliwa Aprili 26, 2014 haiandikiki kwa maana kuwa muda huo hauwezi kutosha kukamilisha mchakato wa kupata Katiba hiyo, vyanzo vimelieleza gazeti la JAMHURI.
Sumaye kumtukana Lowassa unajidhalilisha, JK umenena
Mpendwa msomaji natumaini hujambo. Wiki hii nimejikuta kwenye mtanziko wa hali ya juu. Zimekuwapo mada nzito nzito, kwa kiwango nashindwa niandike juu ya ipi na kuacha ipi. Hata hivyo, mambo matatu nitayagusia. Mchango wa Waziri Mkuu wa zamani bungeni, Edward Lowassa, Mkutano wa Waziri Mkuu wa zamani Frederick Sumaye na hotuba ya mwaka ya Rais Jakaya Kikwete kuhusiana na Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kikwete anastahili pongezi
Wiki iliyopita ilikuwa na matukio makuu mawili. Tukio la kwanza ni Alhamisi, ambapo Rais Jakaya Kikwete alihutubia Bunge. Alisema bayana kuwa alikwenda bungeni kuzungumza suala moja tu la msingi, ingawa alichomekea mengine. Suala hili ni mustakabali wa Tanzania ndani ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).
Gesi yabadili utamaduni Mtwara
Wiki hii Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Eliakim Maswi (pichani), amefanya ziara ya siku tatu mkoani Mtwara kuangalia maendeleo ya ujenzi wa bomba la gesi. Nimepata fursa ya kuwamo kwenye ziara hii. Nimeshuhudia mengi.
MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE
Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (6)
Wiki iliyopita tulikuletea sehemu ya tano ya mtiririko wa maandiko ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere juu ya Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania. Katika kitabu alichokiandika mwaka 1994, Mwalimu alisema: “Ati Chama hakiwezi kupinga Bunge lake, lakini kwa mantiki ya ajabu ajabu wabunge wanaweza kupinga chama chao! Hiyo ndiyo demokrasia halisi ya mageuzi. Nilirudi Butiama nikalipa ada yangu ya CCM na nikaandika utenzi wa Tanzania Tanzania!” Endelea…
Jukumu la kueleza taarifa hii ya Serikali katika Halmashauri Kuu ya Taifa aliachiwa Waziri wa Sheria na Mambo ya Katiba, Mheshimiwa Samuel Sitta. Baadaye, baada ya kikao nilimtafuta Ndugu Sitta, nikampa pole kwa kupewa jukumu la kueleza jambo ambalo halielezeki.