Latest Posts
Chadema ‘Kimewaka’
Chimbuko migogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unasababishwa migongano wa kupata madaraka ndani ya chama hicho, JAMHURI limebaini
Imelezwa kuwa mtafaruku uliotokea mwishoni mwa wiki na kusababisha kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Arusha wa Chadema kwa muda usiojulikana ni mgongano wa kutafuta madaraka ndani ya chama hicho.
Wakimbia makazi kukwepa operesheni okoa
Siku chache baada ya maofisa wanaoendesha Operesheni Okoa Mazingira iliyofanyika katika Kijiji cha Usinge wilayani Kaliua, kutuhumiwa kumuua, Kipara Issa (39), kwa tuhuma za kumiliki silaha kinyume na sheria, baadhi ya wanaume katika kijiji hicho wamelazimika kuzikimbia familia zao kwa hofu ya kukamatwa na maofisa hao.
Vuta nikuvute Kituo cha Mabasi Ubungo
Wadau mbalimbali wanaotoa huduma za aina tofauti katika Kituo cha Mbasi yaendayo mikoani na nje ya ncha cha Ubungo jijini Dar es Salaam wamehushutuma uongozi wa kituo hicho kwa kile walichokiita kuwa ni utaratibu mbovu wa uendeshaji.
MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE
Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (4)
Huu ni mtiririko wa maandishi yaliyomo kwenye kitabu cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania kilichoandikwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwaka 1994. Sehemu iliyopita, Mwalimu alisema, “Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili – ya Zanzibar na ya Tanganyika – kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar. Wapendao Utanganyika watakuwa wazalendo zaidi, badala ya kuwa wasaliti, wakiazimia Afrika ya Mashariki iliyoungana kuwa Nchi Moja, kuliko Tanzania iliyotengana ikawa nchi mbili.” Endelea…..
Siku ya pili yake tarehe 15:8:1993, Wabunge wenye hoja yao, na wengine zaidi, waliomba tena kuja Msasani ‘Tunywe chai’. Na baada ya mazungumzo nao ilikuwa ni dhahiri kabisa kwangu, kwamba hata kama hawakuondoa hoja yao, (wala mimi sikuwaomba waiondoe), wataitumia kutoa dukuduku zao tu; hawataitumia kung’ang’ania kudai Serikali ya Tanganyika.
Nishati na Madini ni Mfano wa kuigwa
Mwishoni mwa wiki iliyopita Wizara ya Nishati na Madini iilitoa taarifa ya utekelezaji wa kipindi cha miezi mitatu iliyopita chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BNR).
JK onesha urais na usiwe mrahisi
Napenda kuchukua fursa hii kumpa pole Rais Jakaya Kikwete kwa majukumu mazito yanayomkabili kwenye uendeshaji wa Serikali, kutokana na mikinzano na vitisho anavyopata kutoka kwa baadhi ya wabunge na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).