JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Chadema ‘Kimewaka’

Chimbuko migogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unasababishwa migongano wa kupata madaraka ndani ya chama hicho, JAMHURI limebaini

Imelezwa kuwa mtafaruku uliotokea mwishoni mwa wiki na kusababisha kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa  Mkoa wa Arusha wa Chadema  kwa muda usiojulikana ni mgongano wa kutafuta madaraka ndani ya chama hicho.

Wakimbia makazi kukwepa operesheni okoa

Siku  chache  baada  ya  maofisa wanaoendesha  Operesheni Okoa Mazingira iliyofanyika katika Kijiji  cha  Usinge wilayani Kaliua, kutuhumiwa kumuua, Kipara Issa (39), kwa tuhuma za kumiliki silaha kinyume na sheria, baadhi ya wanaume katika kijiji hicho wamelazimika kuzikimbia familia zao kwa hofu ya kukamatwa na maofisa hao.

Vuta nikuvute Kituo cha Mabasi Ubungo

 

Wadau mbalimbali wanaotoa huduma za aina tofauti katika Kituo cha Mbasi yaendayo mikoani na nje ya ncha cha Ubungo jijini Dar es Salaam wamehushutuma uongozi wa kituo hicho kwa kile walichokiita kuwa ni utaratibu mbovu wa uendeshaji.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

 

Uongozi Wetu na  Hatima ya Tanzania (4)

Huu ni mtiririko wa maandishi yaliyomo kwenye kitabu cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania kilichoandikwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwaka 1994. Sehemu iliyopita, Mwalimu alisema, “Kwa kweli hata kesho Nchi za Afrika ya Mashariki zikiamua kuungana, na Tanzania ikawa ni mshiriki, naamini kuwa ni rahisi zaidi kushirikisha Tanzania yenye Serikali Mbili – ya Zanzibar na ya Tanganyika – kuliko Tanzania yenye Serikali Mbili, ya Tanzania na ya Zanzibar. Wapendao Utanganyika watakuwa wazalendo zaidi, badala ya kuwa wasaliti, wakiazimia Afrika ya Mashariki iliyoungana kuwa Nchi Moja, kuliko Tanzania iliyotengana ikawa nchi mbili.” Endelea…..

Siku ya pili yake tarehe 15:8:1993, Wabunge wenye hoja yao, na wengine zaidi, waliomba tena kuja Msasani ‘Tunywe chai’. Na baada ya mazungumzo nao ilikuwa ni dhahiri kabisa kwangu, kwamba hata kama hawakuondoa hoja yao, (wala mimi sikuwaomba waiondoe), wataitumia kutoa dukuduku zao tu; hawataitumia kung’ang’ania kudai Serikali ya Tanganyika.

Nishati na Madini ni Mfano  wa kuigwa

 

Mwishoni mwa wiki iliyopita Wizara ya Nishati na Madini iilitoa taarifa ya utekelezaji wa kipindi cha miezi mitatu iliyopita chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa sasa (BNR).

JK onesha urais na usiwe mrahisi

Napenda kuchukua fursa hii kumpa pole Rais Jakaya Kikwete kwa majukumu mazito yanayomkabili kwenye uendeshaji wa Serikali, kutokana na mikinzano na vitisho anavyopata kutoka kwa baadhi ya wabunge na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM).