JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Natamani serikali ya China ingekuwa Tanzania

Waswahili siku zote husema adaa ya mja kunena, muungwana ni kitendo. Serikali ya China ni mfano mzuri wa kuigwa kwa jinsi inavyosimamia sheria, sera na taratibu zake kwa vitendo. Natamani serikali ya China ingekuwa Tanzania ili, pamoja na mambo mengine, ishughulikie kwa vitendo watumishi wanaotumia vibaya madaraka na ofisi za umma.

Utaifa hauna dini (1)

 

Wakoloni, hasa Waingereza, walikuwa na ubaguzi wa hali ya juu. Miongoni mwa raia wao walikuwapo walioitwa raia halisi (British nationals), na raia watawaliwa (British subjects).

Dk. Hoseah aomba majina ya walioficha mabilioni Uswisi

 

*Asema Takukuru haizuii watu kujenga mahekalu

*Wadau wataka wanaothibitika kula rushwa wauawe

 

Ujasiri na ushirikiano wa dhati vimetajwa kuwa ni miongoni mwa nyenzo thabiti, zinazoweza kuongeza ufanisi katika mapambano dhidi ya vitendo vya rushwa nchini.

 

Rushwa uchaguzi CCM inatisha

Uchaguzi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) unaelekea ukingoni. Tayari viongozi wa nafasi mbalimbali kuanzia ngazi ya mashina hadi Taifa wameshapatikana. Tunawapongeza waliochaguliwa. Lakini pongezi zetu za dhati kwa kweli tunazielekeza kwa wale waliochaguliwa bila kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Hapendwi mtu UK, hata awe waziri

 

Tabia ya Waingereza kuzijua na kuzitetea haki zao, inanipa faraja kubwa sana wana-Jamhuri wenzangu. Watu wakubwa wamejikuta wanaanguka kwa mambo yanayotokana na kushindwa kuheshimu wadogo. Mfano wake ni Mnadhimu Mkuu wa Serikali, Andrew Mitchell, anayetota matatani kwa kuwaita polisi wanaoshika lindo kwenye Ofisi za Waziri Mkuu pale Downing Street kuwa ni “kajamba nani” tu.

Yah: Tujiulize, maendeleo yaondoe utamaduni wetu?

Wanangu, wakati wa ujana wetu kulikuwa na starehe nyingi ambazo leo nyie hamuwezi kuzifanya kwa gharama yoyote ile labda mjigeuze na kuomba kwa Mwenyezi Mungu miaka irudi nyuma na mpate nafasi ya kufaidi kama tulivyofaidi sisi.