JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Afadhali ya ‘ngangari’ kuliko ‘magwanda’ haya (1)

Si siri kuwa tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi nchini, mambo si shwari. Amani na utulivu wa nchi yetu vimetikisika. Nadiriki kusema hivi kwa sababu, tangu Uchaguzi Mkuu wa kwanza uliofanyika mwaka 1995, amani na utulivu vimekuwa vikiyumba kila kukicha.

TanzaniteOne yachimba, yasafirisha tanzanite bila leseni halali

Kampuni ya TanzaniteOne Ltd inayochimba madini ya tanzanite katika eneo la Mererani mkoani Manyara, inaendelea kuchimba madini hayo licha ya leseni iliyoiruhusu kufanya kazi hiyo kwisha muda wake, JAMHURI imeelezwa. Kampuni hiyo kutoka Afrika Kusini, inamiliki mgodi huo kwa asilimia…

TanzaniteOne yachimba, yasafirisha tanzanite bila leseni halali

Kampuni ya TanzaniteOne Ltd inayochimba madini ya tanzanite katika eneo la Mererani mkoani Manyara, inaendelea kuchimba madini hayo licha ya leseni iliyoiruhusu kufanya kazi hiyo kwisha muda wake, JAMHURI imeelezwa.

Ahadi hizi za Kikwete zinatekelezeka?

Wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu mwaka 2010, mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, alitoa ahadi nyingi mno.

Kikwete apendelea familia yake CCM

 

*Ahakikisha wanne wa familia yake wanapita

*Naye akichaguliwa uenyekiti atakamilisha ‘The Kikwete 5’

*Mwanae mwingine ni Mjumbe Chipukizi Taifa

*NEC ijayo itakuwa ya Baba, Mama na Watoto (BMW)

 

Mjadala mkali umeibuliwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, ukihusisha familia ya Kikwete kuwa na wagombea watano wa nafasi tofauti ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Tayari majina manne yameshapitishwa, huku jina la Rais Jakaya Kikwete likisubiriwa kuwa la tano wakati atakapojitokeza kuwania nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa.

 

Mkakati wa 2015 waiva

Makundi ya kuhasimiana ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), yameendelea kukiburuza chama hicho kwa kuimarisha mkakati wa kupachika wagombea wao kwenye nafasi mbalimbali ikiwamo Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC-CCM).