Latest Posts
Hotuba iliyowazima wabunge mafisad
Bunge linanuka rushwa. Baadhi ya wabunge wanapokea rushwa ili kutetea maslahi ya wanaowatuma. Lakini wapo wabunge jasiri walioamua kupambana na wenzao wala rushwa kama inavyothibitishwa na Hotuba ya Msemaji wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Wizara ya Nishati na Madini,…
Bahanuzi aleta ladha katika soka
LICHA ya Tanzania kumudu kulibakiza nyumbani Kombe la Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati – maarufu zaidi kwa jina la Kagame – mshambuliaji wa Simba Sports Club, Felix Mumba Sunzu ameibuka kuwa galasa huku mashabiki wakijiuliza kuhusu sifa zinazofanya timu hiyo iendelee kumng’ang’ania.
Muhongo, Maswi wanatisha
*Gharama za kuunganisha umeme zakuna wengi
*Migodi yote si hiari tena kulipa kodi ya mapato
*Afuta mashangingi ya bure, vigogo watakopeshwa
*Mnyika, Selasini wawanyoosha wabunge wala rushwa
Wananchi wengi wameeleza kufurahishwa na msimamo wa uongozi mpya wa Wizara ya Nishati na Madini wa kuwapunguzia wananchi ukali wa gharama za kuunganisha umeme, kufuta ununuzi wa mashangingi na kuwabana wenye migodi mikubwa kuanza kulipa kodi ya mapato.
Haya ndiyo mambo murua yanayoliliwa na Watanzania
Wizara ya Nishati na Madini imetangaza kupunguza gharama za kuunganishia wateja wake umeme. Gharama hizo zimepungua kwa wastani wa asilimia 30 na 77. Uamuzi huo ulitangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, bungeni mwishoni mwa wiki.
Biashara za sasa zinahitaji u-sasa
Wakati baba yangu mzazi akifariki katikati ya miaka ya 1990, alikuwa mmoja wa wafanyabiashara waliokuwa wakipanda kwa kasi kubwa kibiashara. Akiwa ameshakusanya uzoefu wa kusafiri kibiashara hadi nchi jirani ikiwamo Malawi, alifariki dunia na kuacha biashara zilizokuwa zimestawi kweli kweli.
Danadana za Sheria ya Habari zitaisha lini?
Wiki iliyopita Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenella Mukangara, amewasilisha bajeti ya wizara yake kwenye mkutano wa Bunge unaoendelea mjini Dodoma. Si nia yangu kujadili bajeti hii inayofikia wastani wa Sh bilioni 19. Na wala sitajadili danadana ilizopigwa bajeti hii, ambayo awali ilikuwa iwasilishwe Julai 18, lakini kwa mshangao ikasogezwa ghafla hadi Agosti 7, kisha kinyemela ikarejeshwa Julai 24.