Latest Posts
TEODENSIA MBUNDA
Mwanamke pekee msaidizi wa waziri
Ni asubuhi na mapema siku ya Jumatano napata wazo la kuonana na Msaidizi wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Teodensia Mbunda.
TBS yajivunia mafanikio yake
Miezi sita iliyotolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara kwa ajili ya kupima utendaji kazi wa Bodi na Manejimenti ya Shirika la Viwango nchini (TBS) imekamilika na hapa Kaimu Mkurugenzi wa TBS, Joseph Masikitiko anaeleza mafanikio yaliyofikiwa kama alivyohojiwa na Mwandishi Wetu, EDMUND MIHALE.
Simba, Sunderland zafunga ‘ndoa’ ya mashaka
Hivi karibuni Tanzania itaanza kufaidika na ushirikiano wa kimichezo na utalii na Klabu ya Sunderland, inayoshiriki Ligi Kuu ya England. Hatua hii inafuata baada ya uongozi wa timu hiyo kutua nchini hivi karibuni na kukutana na uongozi wa Serikali kupitia Bodi ya Utalii nchini.
NUKUU ZA WIKI
Julius Nyerere: Serikali imiliki mashirika nyeti
“Mashirika ya msingi na nyeti kwa maendeleo ya taifa kama bandari, reli, posta na simu, nishati na mabenki ya umma yaliyopo, yaendelee kumilikiwa na dola. Wananchi wataweza kuuziwa sehemu ya hisa katika mashirika hayo na mashirika haya yanaweza kuingia ubia na makampuni binafsi, mradi tu kwa uwiano unaolifanya shirika kuendelea kuwa la dola.”
Mayweather avuna Sh bilioni 67 kwa dakika 36
Bondia maarufu duniani, Floyd Mayweather (36) atalipwa dola milioni 41.5 za Marekani (Sh bilioni 67.23), baada ya kumshinda Saul ‘Canelo’ Alvarez (23). Hili ni pambano la 45 kwa Mayweather akiwa ameshinda yote.