JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Utajiri wa Loliondo na laana yake (2)

 

Mfululizo huu wa makala kuhusu Loliondo ulianza wiki mbili zilizopita. Kwenye toleo la mwisho, tuliishia kwenye kipengele kinachopingana na propaganda za uongo kwamba Serikali imechukua ardhi ya vijiji. Mwandishi anasema baadhi ya madiwani na NGOs zimetumiwa kueneza uongo huo kwa maslahi yao ya kisiasa na kiuchumi. Endelea.

Mwalimu Nyerere alijua ujio wa Obama tangu mwaka 1967

Mwaka huu pekee, Tanzania imepokea marais wa mataifa mawili makubwa yanayoongoza kwa uchumi imara duniani. Rais Xi Jinping wa China alikuwa wa kwanza, na baadaye amefuatiwa na Rais Barack Obama wa Marekani. Ujio wa viongozi hao, pamoja na kauli za kwamba wanataka kufungua milango ya kushirikiana kiuchumi, ni ukweli ulio wazi kwamba Tanzania imeendelea kurusha ndoana ya kuomba misaada. Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere, katika hotuba yake ya Februari 5, 1967 jijini Dar es Salaam, alieleza athari za nchi kuwa omba-omba. Sehemu hii ya hotuba inapatikana kwenye kitabu chake cha Ujamaa ni Imani (2). Endelea.

MISITU & MAZINGIRA

Misitu ya Asili na Maendeleo ya Jamii Tanzania (4)

Toleo lililopita, Dk. Kilahama alieleza umuhimu wa viongozi wa vijiji na jamii kuhakikisha wanapata manufaa kutokana na misitu, hasa ya asili. Akasisitiza umuhimu wa uongozi bora na imara katika vijiji na vikundi vya kijamii. Endelea.

Kumbe ndiyo maana Marekani inachukiwa!

Umasikini ni kitu kibaya mno. Haya ndiyo yaliyonijia kichwani kabla na wakati wote ziara ya Rais Barack Obama wa Marekani.

Mengi ameonesha njia, wengine waige

Kabla ya kuzungumzia mada ya leo, ninapenda kuwashukuru wasomaji wote wa Safu hii walionipigia simu, kunitumia ujumbe mfupi wa maneno (SMS) na e-mail, baadhi wakinipongeza, kunishauri na wengine wakinikosoa kuhusu makala niliyoandika wiki iliyopita, iliyobebwa na kichwa cha habari, “Watanzania na imani potofu ziara ya Obama.” Nimejifunza mengi kutoka kwao.

Vidonda vya tumbo na hatari zake (4)

Katika sehemu ya tatu ya makala haya, Dk. Khamis Zephania alieleza maana na sababu za fumbatio, vidonda vya umio na jinsi vidonda vya tumbo vinavyotokea. Sasa endelea kumfuatilia katika sehemu hii ya nne…