JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

Magufuli amvimbia Pinda

Kuna kila dalili kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli, amekataa au kushindwa kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutokana na kilichoelezwa kuwa kuyatekeleza ni kuvunja sheria ya usalama barabarani na kanuni zake, hivyo yeye hayuko tayari kufanya hivyo.

Meya Mwanza, madiwani wapimana ubavu

  • Mabishano, matusi vyakwamisha kikao
  • Polisi washindwa, Meya atumia mabaunsa

Ni dhahiri kuwa sasa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza hapakaliki. Mgogoro baina ya Meya Henry Matata na madiwani watatu aliowafukuza, unazidi kufukuta na kuhatarisha maendeleo ya wananchi.

Mwigamba ni bomu linalosubiri wakati

Mwaka 2008 nilisoma makala aliyoandika Samson Mwigamba. Nilipoisoma makala hayo nilibaini kuwa Mwigamba ni bomu linalosubiri wakati, lakini watu waliokuwa wamepofushwa na mapenzi dhidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) waliishangilia makala ile.

PPF yafafanua michango ya zamani

Mfuko wa Pensheni wa Mashirika ya Umma (PPF) umewatoa wasiwasi wafanyakazi wa mashirika ya umma waliochangia tangu mwaka 1978, kwa michango isiyoonekana kwenye mtandao wa mfuko huo.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

 

Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania (5)

Huu ni mtiririko wa maandishi yaliyomo kwenye kitabu cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania kilichoandikwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mwaka 1994. Sehemu iliyopita, Mwalimu alisema, “Ni vigumu kuelewa kwa nini watu walio tayari kuwabebesha wananchi mzigo wa SeIikali tatu za kudumu, wanahofu gharama za kura ya maoni ya mara moja! Na kama viongozi wetu ni wapumbavu kiasi cha kwamba hawawezi kutunga swali “Je, unataka Serikali tatu?” Au “Je, unataka Serikali ya Tanganyika?” Kazi hiyo wangeweza kuwaachia wataalamu wenye uwezo zaidi.” Endelea…..

Kwa kutambua kwamba Bunge linafanya uamuzi yake kwa njia ya kura baada ya mijadala ya wazi, Serikali iliona kwamba hoja yoyote kati ya hizi ingewasilishwa bungeni, ingeweza kuligawa Bunge, kukigawa chama chetu na kuwagawa wananchi katika suala zito kama hili la Muundo wa Muungano.

Operesheni Tokomeza ilistahili, waliofanya uhuni waadhibiwe

Wiki iliyopita Bunge limetoa maelekezo kwa Kamati ya Maliasili na Utalii kuchunguzia utekelezaji na mwenendo wa Operesheni Tokomeza. Operesheni hii imeendeshwa kwa makusudi kudhibiti majangili waliokuwa wakiua tembo kwa kasi ya ajabu na kutishia uwepo wa tembo nchini. Wabunge wamelalamika kuwa askari walioendesha operesheni hii walikosa uaminifu.