JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Latest Posts

CCM wachimba umaarufu wa CHADEMA Moshi

MADIWANI wa Manspaa ya Moshi, mkoani Kilimanjaro wamemwandikia barua Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakimuomba akubali kusaini makubaliano ya mkopo wa Sh bilioni 19 za ujenzi wa kituo kipya cha mabasi yaendayo mikoani na nje ya nchi kilichopo eneo la Ngangamfumuni mjini Moshi.

Unahitaji ‘gia’ ya uvumilivu kumudu biashara

Ninaandika makala haya baada ya kumtembelea Frank Mwaisumbe na kubadilishana naye mawazo, wiki mbili zilizopita. Ni mfanyabiashara aliyepo mjini Iringa anayemiliki kampuni ya uwakala wa safari za anga iitwayo Getterland Company Limited. Mwaisumbe pia ni mmoja ya waasisi wa Shirika la Mindset Empowerment linaloendesha mashindano ya mbio za Ruaha Marathon.

Wao na mashangingi, masikini na sakafu

Rais Paul Kagame wa Rwanda alipotwaa madaraka, miongoni mwa “uamuzi mgumu” wa awali aliouchukua ni kuhakikisha anapunguza matumizi yanayosababishwa na magari ya umma. Akayakusanya kwa wingi. Akayaweka uwanjani. Akapewa orodha ya maofisa na watumishi wanaostahili kukopeshwa magari. Akawaagiza waende uwanjani- kila mmoja achague analotaka. Akahakikisha aliyechagua gari anakopeshwa-linakuwa mali yake. Huduma za mafuta na matengenezo zikaandaliwa utaratibu kwa kila gari na kwa muda maalumu.

fasihi fasaha

Tunakubali rushwa ni adui wa haki? (4)

Ni miaka 17 sasa tangu Tume ya Kero ya Rushwa ilipotufahamisha mianya na sababu za kuwepo rushwa, wala rushwa na njia za kuitokomeza. Lakini kilio kikubwa cha madhara ya rushwa bado kinasikika kutoka kwa wananchi.

FIKRA YA HEKIMA

Tunahitaji rais dikteta mwenye uzalendo

Jumamosi iliyopita wakati jua likielekea kuchwea, nilihisi faraja kuandaa makala hii kutoa changamoto kwamba nchi yetu sasa inahitaji kuwa na rais dikteta lakini aliye mzalendo. Dikteta ni mtu anayetawala nchi kwa amri zake bila kushauriwa, au anayetaka analosema litekelezwe bila kupingwa, na mzalendo ni mtu anayependa nchi yake kiasi cha kuwa tayari kuifia.

Ni ujinga CHADEMA kupinga uzazi wa mpango – (2)

Amani Golugwa amendelea kudai kuwa wasomi wengi wameshangazwa na kauli ya Rais Kikwete ya kuwataka Watanzania wafuate uzazi wa mpango. Huo ni uzushi ambao CHADEMA ni kawaida yao.