Na Jeshi la Polisi, Dodoma

Kamishna wa Fedha na Lojistiki wa Jeshi la Polisi CP Liberatus Sabas, akimpitisha Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, akiwa ameambatana na Makamishna wengine kwenye maendeleo ya ujenzi wa nyumba za makazi ya askari unaoendelea Mkoani Dodoma.

Mpaka sasa jumla ya maghorofa sita yanajengwa kwa pamoja ambapo ujenzi huo umefikia katika hatua mbalimbali huku kila ghorofa moja ikiwa na sakafu (floor) nne.

Tukio hilo limefanyika leo Julai 15,2025 wakati Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Camillus Wambura, akifanya ukaguzi wa majenzi unaoendelea mkoani humo.