JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Archives

Vituo vya mafuta vinaiba kodi mchana kweupe

Mzee Ali Hassan Mwinyi alipata kusema maneno haya: “ Tanzania ni sawa na kichwa cha mwendawazimu.” Maneno haya aliyasema kwa maana kwamba kichwa cha mwendawazimu kila anayejifunza kunyoa hufanyia hapo mazoezi. Wiki iliyopita nilikuwa Nairobi , Kenya ambako nilikuwa na mafunzo ya wiki zaidi ya mbili. Nikiwa huko kwa mshangao nikakuta Tanzania inamwagiwa sifa.