OR – TAMISEMI

Serikali kupitia bajeti yake ya mwaka 2025/2026 inakusudia kuzifanyia ukarabati shule zote kongwe za msingi na sekondari zilizochakaa ili kuzirejesha katika mwonekano wake wa awali.

Kauli hiyo imetolewa leo Juni 04, 2025 bungeni Jijini Dodoma na Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI (AFYA) Mhe. Dkt. Festo Dugange wakati akijibu maswali ya Waheshimiwa Wabunge katika kipindi cha maswali na majibu kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Naibu Waziri Dkt. Dugange amesema tayari OR – TAMISEMI imeianisha shule zote kongwe na chakavu zinazohitaji ukarabati wa haraka na imefanya tathmini ya uhitaji wa fedha kwa ajiri ya ukarabati wa shule hizo awamu kwa awamu.

Amesema katika bajeti ya Serikali ijayo shule zote zilizo ainishwa zimepewa kipaumbele ambapo zitakarabatiwa awamu kwa awamu kulingana na kiasi cha fedha kutoka Serikali Kuu pamoja na upatikanaji wa fedha kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri.