Serikali ya Uingereza imetangaza mipango ya kukabiliana na biashara ya upasuaji kwa ajili ya kuboresha muenekano ikiwemo kuongeza makalio, kuongeza ukubwa wa viungo kama midomo na kuondoa makunyazi usoni.

Hatua hizo zinadhamiria kuwalinda watu walioko chini ya umri wa miaka 18 na kuhakikisha kuwa ni maafisa wa afya waliofuzu tu kuhudumu Uingereza watakaoruhusiwa kutoa huduma hizo za kunakshi urembo.

Kumekuwa na wasiwasi kuwa watu wanafanyiwa upasuaji na kupewa dawa katika mazingira yasiyo salama ikiwemo majumbani, kwenye mahoteli na kiliniki za muda na hivyo kuhatarisha maisha yao.