Chama cha Mapinduzi (CCM) kupitia Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo, CPA Amos Makalla, kimetangaza rasmi majina ya wagombea watakaoshiriki Uchaguzi Mkuu wa 2025 kwa nafasi za Ubunge wa Majimbo, Viti Maalum na Ujumbe wa Baraza la Wawakilishi.

CPA Makalla amesema uteuzi huo, uliofanywa na Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, umehusisha majimbo 272 upande wa Tanzania Bara na umehitaji umakini mkubwa kutokana na wingi wa maombi ya wagombea.

“Majimbo zaidi ya elfu tano yalipokea maombi ya wagombea,Kazi hii ilikuwa kubwa na ilihitaji umakini mkubwa ,Kwa wale ambao hawajapata uteuzi, tunawaomba waendelee kuwa watiifu kwa chama kwani bado CCM inawathamini,” amesema CPA Makalla.

  1. Mhe. Mrisho Mashaka Gambo : Arusha Mjini
  2. Mhe. Emanuel Ole Shangai : Ngorongoro
  3. Mhe. Mohamed Lujuo Moni : Chemba
  4. Mhe. Nicodemus Maganga : Mbogwe
  5. Mhe. Justine Nyamoga : Kilolo
  6. Mhe. Stephen Byabato : Bukoba Mjini
  7. Mhe. George Ndaisaba Ruhoro : Ngara
  8. Mhe. Zuberi Mohammed Kuchauka : Liwale
  9. Mhe. Pauline Gekul: Babati Mjini
  10. Mhe. Flatey Maasai : Mbulu Vijijini
  11. Mhe. Christopher Ole Sendeka : Simanjiro
  12. Mhe. Vedastus Matayo Manyinyi : Musoma Mjini
  13. Mhe. Luhaga Joelson Mpina : Kisesa
  14. Mhe. Godwin Kunambi : Mlimba
  15. Mhe. Geoffrey Mwambe : Masasi
  16. Mhe. Cecil Mwambe : Ndanda
  17. Mhe. Anjelina Mabula : Ilemela
  18. Mhe. Mansour Shanif Hirani : Kwimba
  19. Mhe. Hassan Zidadu Kungu : Tunduru Kaskazini
  20. Mhe. Iddi Mpakate : Tunduru Kusini
  21. Mhe. Iddi Kassim Iddi : Msalala
  22. Mhe. George Mwenisongole : Mbozi
  23. Mhe. Seif Hamisi Gulamali : Manonga
  24. Mhe. Omar Shekilindi : Lushoto
  25. Mhe. Januari Makamba : Bumbuli
  26. Mhe. Alfred Kimea : Korogwe Mjini
  27. Mhe. Twaha Mpembenwe : Kibiti