BALOZI SOKOINE AKUTANA NA WATANZANIA UBELGIJI

Balozi wa Tanzania nchi Ubelgiji Mh:Edward Joseph Sokoine katikati akiwa na baadhi ya watanzania waliofika jana kwenye kikao cha kusikiliza na kutafutia ufumbuzi kero za watanzania wanaishi mbali na Tanzania. {Picha zote na Maganga One Blog} 
Kiongozi wa Watanzani kitongoji cha Antwerpen nchini Ubelgiji ndugu Joseph Makani akimkaribisha Mh;Balozi na maafisa Ubalozi alioambana nao hapa jana,kutoka kushoto ni Afisa Ubalozi ndugu Shoo na upande wa kulia ni afisa ubalozi ndugu Juma Salum.Kikao kilikwenda vizuri kwani kila mmoja alipewa fursa ya kuuliza maswali. {picha zote na Maganga One Blog} 
Afisa Ubalozi ndugu Juma Salum{kulia}akitoa ufafanuzi wa swali aliloulizwa kuhusu maswala ya hati za kusafiria pindi mtu anapotaka kurudi nyumbani,alielezea kwa kirefu taratibu zinazotakiwa kufuatwa ili mtu kuepuka usumbufu. 
Mh:Balozi akimsikiliza mmoja wa watanzania ndugu Omari Songambele {hayupo pichani}aliyetaka ufafanuzi kuhusu Uraia Pacha. 
Baadhi ya kina mama wa Kitanzania na nchi jirani walihudhuria mkutano uliowakutanisha na Balozi Sokoine 
Na kwa upande wa kina baba nao walijumuika kwa wingi hapo jana kusikiliza na kutoa maoni kuhusu nchi yao 
Mwenyekiti wa Watanzania nchini Ubelgiji ndugu Mwasha akijitambulisha kwa Mh:Balozi kabla ya kikao hakijaanza rasmi. 
Afisa ubalozi wa Tanzania ndugu Juma Salum,jana alipata nafasi nzuri ya kuyajibu vizuri maswali ya watanzania. Pichani akiendelea kufafanua jinsi ofisi ya balozi inavyofanya kazi zake vyema na kuwasaidia watanzania kwa hali na mali pindi wanapohitaji msaada kwenye ofisi za ubalozi. 
Mmoja wa Watanzania ambaye anaishi nje ya nchi na amefaikiwa kuzaa na mzungu,Pichani wakimsikiliza Mh:Balozi 
Pichani baadhi ya Watanzania wakimsikiliza Mh:Balozi 
Pichani baadhi ya Watanzania wakimsikiliza Mh:Balozi 
Mh:Balozi Sokoine akiwasisitiza Watanzania kuwekeza na kupeleka wawekezaji nyumbani 
Afisa balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji ndugu Shoo akiwaeleza watanzania Fursa za Hisa zitokanazo na mabenki makubwa nchini Tanzania na jinsi ya kujiunga nazo 
Afisa Ubalozi wa Tanzania nduguKabakati nae aliongea na watanzania kuhusu uwekezaji katika sekta mbalimbali,pichani alitoa ufafanuzi wa maswala ya umiliki wa ardhi na mashamba 
Afisa ubalozi na Kanali mstaafu akiwashauri Watanzania kutokusahau walikotoka na kuwasisitiza kuwekeza nyumbani,kutovunja sheria za nchi wanazoishi 
Afisa ubalozi na Kanali mstaafu akiwashauri Watanzania kutokusahau walikotoka na kuwasisitiza kuwekeza nyumbani,kutovunja sheria za nchi wanazoishi 
Watanzania,Wasomali,Warundi , Wacongo na nchi nyingine za jirani kuizunguka Tanzania walihudhuria mkutano wa Balozi wa Tanzania Mh:Balozi Sokoine hapo jana. 
Maganga One Blogger akiwa na maafisa ubalozi wa Tanzania wakibadilishana mawazo 
Maganga One Blogger alipata fursa ya kuongea na Mh:Balozi na kumueleza changamoto za Watanzania ughaibuni,Mh:Balozi Sokoine aliahidi kuwasaidia Watanzania kadri atakavyoweza na kutatua kero zao. 
Mh:Balozi Sokoine akiagana na Omary Songambele mara baada ya kikao kumalizika hapa jana.pembeni mwa balozi ni Dulla Criss Cross mmoja wa viongozi wa Antwerpen 
Shabiki namba moja wa Simba ughaibuni ndugu Nyambi kushoto akiwa na dada wa Kitanzania wakipata picha ya kumbukumbu 
Kutoka kushoto ni Afisa Balozi na kanali mstaafu,ndugu Omary Songambele,Mchezaji wa zamani wa timu ya Taifa Kassim Manara,Afisa ubalozi ndugu Kabakati na Mh:Balozi Edward Sokoine hapo jana jijini Antwerpen katika kikao cha kuzungumzia maendeleo ya nchi ya Tanzania.