CHADEMA YATANGAZA KUSITISHA KAMPENI ZA UCHAGUZI WA WABUNGE

Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ametangaza kusitishwa kwa kampeni zauchaguzi wa Wabunge wa  chama hicho zinazoendelea, ili kushiriki maziko ya Mzee Kingunge Ngombale Mwiru.
Mzee Kingunge alifariki juzi kwenye Hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa majeraha ya kung’atwa na mbwa wake nyumbani kwake.
Mzee Kingunge anazikwa leo Februari 5, katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam.