Barcelona imebanwa mbavu katika harakati zake za kuendelea kujivunia alama za kukalia kilele cha msimamo wa Ligi Kuu Spain, baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Las palmas.

Barcelona ambao walikuwa ugenini, walianza kupata bao la kwanza kwa njia ya mpira wa faulo kupitia Lionel Messi (21′), na baadaye Las Palmas wakasawazisha kwa njia ya tuta kupitia kwa Jonathan Calleri (48′).

Licha ya sare hiyo, Barcelona bado wamekalia usukani wa ligi kwa alama 66 mpaka sasa

By Jamhuri