Leo ni leo, asemaye kesho ni mwongo. Timu maarufu za soka barani Ulaya, Manchester United na Real Madrid, leo zinatinga uwanjani kumenyena katika kinyang’anyiro cha Mabingwa wa Ulaya (UEFA). Manchester United inatinga katika mtanange huo ikiwa inajivunia mshambuliaji wake, Christiano Ronaldo, huku Real Madrid ikimtegemea zaidi Van Persie.

By Jamhuri