Baada ya kwenda sare ya bao 1-1 na Iran usiku wa jana, timu ya taifa ya Ureno sasa itakutana na Uruguay katika mchezo unaofuata ya 16 bora kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi.

Mchezo huo ulimazika kwa sare hiyo huku nyota na nahodha wa Ureno, Cristiano Ronaldo akikosa penati ambayo ingeweza kuiongezea alama timu yake.

Uruguay anayoichezea nyota Luis Suarez sasa itakuwa inakipiga na Ureno baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Urusi.

Wakati huo Spain iliyokwenda sare ya mabao 2-2 na Morocco itakuwa inakipiga dhidi ya Russia iliyopokea kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Uruguay.

Mechi hizo za mkondo wa hatua ya 16 bora zitaanza kuwaka moto Juni 30 kwa mujibu wa ratiba ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

By Jamhuri