RAIS WA AFRIKA KUSINI, JACOB ZUMA ANG’ATUKA MADARAKANI

Jacob Zuma, ametangaza kujiuzulu nafasi yake ya Urais

Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma amejiuzulu baada ya shinikizo nyingi kutoka kwa chama chake.

Kapitia hotuba yake iliyopeperushwa kwa njia ya televisheni alisema anajiuzulu mara moja lakini akaongeza kuwa hakubaliani na uamuzi wa chama cha ANC.

Chama cha ANC kilikuwa kimemuambia aondoke madarakani au akabiliwe na kura ya kutokuwa na imani naye bungeni.

Zuma mwenye umri wa miaka 75 amekuwa akikabiliwa na shinikizo za kumtakja ampe nafasi mamamu wake Cyril Ramaphosa, ambaye ndiye sasa kiongozi mpya wa chama.

Bw Zuma ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2009, amekumbwa na shutuma nyingi za ufisadi.

Mapema Jumatano, polisi walivamia nyumba ya familia tajiri ya Gupta ambayo Zuma ana uhusiano wa karibu nayo.

Zuma alijiuzulu kwa njia gani?

Alianza hotuba kwa kucheka na kufanya mzaha na waandishi wa hahari.

Baada ya kuwashukuru wale ambao amefanya kazi nao kwa miaka kadhaa, Bw Zuma alisena kuwa ghasia na migawanyiko ndani ya ANC imesabisha ajiuzulu.

“Hakuna maisha itapotea kwa sababu yangu wala ANC haiwezi kugawanyika kwa sababu yangu. Kwa hivyo nimefikia uamuzi wa kujiuzulu kama rais wa nchi mara moja,” alisema

“Licha ya kutokubaliana na uamuzi wa chama changu, siku zote nimekuwa mwanachama mwenye nidhamu wa ANC.

“Ninapoondoka, niataendelea kuwatumikia watu wa Afrika Kusini sawa na ANC, chama ambacho nimekitumikia maisha yangu yote.”

SOURCE: BBC