Kikosi cha timu ya Wabunge wa Tanzania wakiwa kwenye picha ya pamoja
Kikosi cha Klabu ya Soka ya Wabunge wa Burundi.

 

KATIKA Michuano ya East Africa Parliamentary Games inayoshirikisha Vilabu vya Mabunge ya nchi za Afrika Mashariki, mechi iliyopigwa katika Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, Timu ya mpira wa miguu Bunge la Tanzania jana iliibuka na ushindi wa bao 3-2 dhidi ya wenzao wa Burundi.

Kwa upande wa Tanzania, mabao yalifungwa na Mohamed Mchengerwa na Yusuf Gogo (aliyetupia mawili), wakati mabao ya Burundi yakifumgwa na Jean Marie Cimpaye na Simon Gakinja kwa mkwaju wa penati.

By Jamhuri