Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asharose Migiro, amewasili na kupokelewa na maelfu ya wananchi waliojitokeza katika viwanja vya mnadani wilayani Karatu mkoani Arusha leo tarehe 3 Oktoba 2025 wakiwa tayari kumsubili na kumlaki Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Rais Dkt. ๐—ฆ๐—ฎ๐—บ๐—ถ๐—ฎ ๐—ฆ๐˜‚๐—น๐˜‚๐—ต๐˜‚ ๐—›๐—ฎ๐˜€๐˜€๐—ฎ๐—ป.

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Migiro ametoa salamu nzuri za ujio wa Dkt. Samia katika viwanja hivyo mda mchache ujao ambaye anatarajiwa kunadi Ilani ya CCM (2025/30) Sera na Ahadi zake ikiwa ni pamoja na kuomba kura.