Zaidi ya watu 200 wamefariki dunia katika mgodi ulioporomoka mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, mamlaka ya waasi imesema.

Mgodi huo, katika mji wa Rubaya, uliporomoka juzi kutokana na mvua kubwa, Lumumba Kambere Muyisa, msemaji wa gavana wa waasi wa eneo la Kivu Kaskazini, aliwaambia waandishi wa habari. Wakati huo, idadi ya vifo haikuwa inajulikana.

Wanawake na watoto walikuwa miongoni mwa wale waliokuwa wakichimba koltani – madini yaliyotumika kutengeneza vifaa vya elektroniki kama vile simu za mkononi na kompyuta – wakati huo.

Msimamizi wa zamani wa mgodi huo aliiambia BBC kwamba eneo hilo halikutunzwa ipasavyo, na hivyo kufanya ajali kuwa rahisi zaidi kutokea na kukwamisha juhudi za uokoaji wakati wa uhitaji.