Takriban watu saba wameuawa wakati ndege ya mizigo ya UPS ilipoanguka ilipokuwa ikipaa kutoka uwanja wa ndege wa Louisville, Kentucky Jumanne jioni, gavana wa jimbo hilo alisema.

Andy Beshear alisema wafanyakazi watatu wa ndege hiyo huenda wakawa miongoni mwa waliofariki baada ya ndege hiyo ya mizigo kulipuka ilipokuwa ikiondoka kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Louisville Muhammad Ali mwendo wa saa 17:15 kwa saa za eneo (22:15 GMT).

Takriban watu wengine 11 wamejeruhiwa wakati ndege hiyo ilipoanguka na kusababisha moshi mwingi angani.

Maafisa wameonya kuwa watu wamepata majeraha “makubwa” katika tukio hilo na kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka.