Askari wa akiba wa Urusi huenda wanatumia “makoleo” kwa mapigano ya “mkono kwa mkono” nchini Ukraine kutokana na uhaba wa risasi, Wizara ya Ulinzi ya Uingereza inasema.

Mwishoni mwa Februari, askari wa akiba walielezea kuwa waliamriwa kushambulia Ukraine “wakiwa na ‘silaha za moto na makoleo’ pekee”, wizara ilisema katika sasisho lake la hivi karibuni la kijasusi.

Walitaja makoleo hayo linalojulikana kama MPL-50.

Kifaa hicho kiliundwa mnamo 1869 na kilikuwa kimebadilishwa kidogo, wizara ilisema.

“Uharibifu wa chombo hicho cha msingi cha toleo la MPL-50 ni simulizi ya kusikitisha haswa nchini Urusi,” wizara hiyo ilisema.

Kuendelea kwa matumizi ya koleo “kama silaha kunaangazia mapigano ya kikatili na ya teknolojia ya chini ambayo yametumika katika vita”, ilisema.

Mmoja wa askari wa akiba alielezea kuwa “hawajajiandaa kimwili wala kisaikolojia” kwa hatua hiyo, taarifa iliongeza.

“Ushahidi wa hivi karibuni unaonesha kuongezeka kwa mapigano ya karibu nchini Ukraine,” ilisema.

“Pengine hii ni matokeo ya amri ya Urusi kuendelea kusisitiza juu ya hatua mbaya ambayo kwa kiasi kikubwa inajumuisha askari wanaotembea kwa miguu walioshuka, na usaidizi mdogo kutoka kwenye mizinga kwa sababu Urusi ina uhaba wa silaha.”

BBC imeshindwa kuthibitisha ripoti hizi kwa uhuru. Wizara haikutoa taarifa za wapi vita hivyo vilikuwa vinafanyika

By Jamhuri