JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Madai ya Nyalandu na majibu ya hoja zake

Katika gazeti la Jamhuri la Jumanne Agosti 19 – 25, 2014 ISSN No. 1821-8156 Toleo No. 150, zilichapishwa taarifa potofu zenye  kichwa cha habari;

KASHFA IKULU;

·    Nyalandu atumia Leseni ya Rais kuua wanyamapori 704 bure,

·    Watakaouawa wamo pia tembo 8, chui 8, Simba 8, ndege,

·    Wauaji ni Wamarekani marafiki wa Waziri wa Maliasili.

Wakenya waingiza mifugo Hifadhi ya Serengeti

Huu ni mpango mahsusi wa kuharibu utalii wa Tanzania na kuvutia watalii katika mbuga ya Maasai Mara nchini Kenya.

JWTZ kurudi tena DRC

Makamanda wa wapiganaji shupavu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) wako mbioni kwenda Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), kuimarisha amani.

Ujio wa Rais Putin balaa

Ulinzi mkali unatarajiwa kuchukua nafasi yake, Rais wa Russia, Vladimir Vladimirovich Putin, atakapozuru Tanzania mapema mwakani kutokana na ‘mbabe’ huyo kuwa na uhasama na Marekani.

Wakati wowote Rais Putin anaposafiri — iwe ndani ya Russia au nje ya nchi — ulinzi wake ni mkali na ulio kamili (almost absolute) kama ule wa Barack Obama wa Marekani.

Kikwete awakoroga wagombea urais

KAULI mbili zilizotolewa na Rais Jakaya Kikwete juu ya kushika wadhifa huo mkubwa nchini, zimewachanganya baadhi ya makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliotangaza na wale wanaotajwa kuwania kumrithi.

Putin anakuja Tanzania

LICHA ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, kusuasua kuthibitisha kuhusu ujio wa Rais wa Russia, Vladimir Putin taarifa za uhakika zinasema kwamba mwamba huyo wa kimataifa atatua nchini Februari, mwakani.