JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

‘Majangili’ 20 hatari

  • JWTZ watisha, maofisa Maliasili 16 wakamatwa
  • Mmoja akutwa anamiliki bunduki 5 za rifle kali
  • Mbunge Mtutura ahojiwa, Nchambi naye atajwa
  • RCO aliahidiwa dola 3,000 akawaachia Waarabu

Operesheni Tokomeza inayoendeshwa chini ya usimamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), imewakamata watumishi kadhaa wa Serikali wanaotuhumiwa kujihusisha na ujangili. Operesheni hiyo inaongozwa na Luteni Kanali A. Sibuti.

JWTZ yafyeka majangili

*Operesheni Tokomeza’ yaanza rasmi

*Inashirikisha, Usalama wa Taifa, Polisi

*Majangili kadhaa hatari yakamatwa

 

JESHI la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limeanza rasmi operesheni ya kuwatokomeza majangili.

Operesheni hiyo iliyopewa jina la Operesheni Tokomeza ilianza rasmi Oktoba 5, mwaka huu ikilenga kuwalinda wanyamapori, hasa ndovu na faru walio hatarini kumalizwa na majangili.

Lindi, Mtwara wapata washirika Norway

Waziri wa Nishati na Madini wa Tanzania, Profesa Sospeter Muhongo, na viongozi wa miji ya Hammerfest na Sandnessjoen nchini Norway, wamekubaliana kuanzisha ushirikiano baina ya miji hiyo na miji ya Lindi na Mtwara.

JWTZ yasafisha M23

*Waasi wakimbilia porini, washindia matunda mwitu

*Zuma atoa makombora yatumike ikiwa wataendelea

*Hatima yasubiriwa Uganda, silaha njaa kuwatoa porini

Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kwa kushirikiana na majeshi washirika ya kimataifa, limewafurumusha askari wote wa kundi la M23 kutoka katika ardhi ya Mji wa Goma, uchunguzi umebaini.

Kamala asisitisa uzalishaji almasi

Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Dk. Diodorus Kamala, ameomba Kampuni ya Petra Diamonds ya nchini humo kuongeza uzalishaji na ubora wa almasi inayozalishwa hapa Tanzania.

M23 wafunga virago

*Kichapo cha JWTZ chawachanganya

*Wengine 1,000 wanaswa, waomba suluhu

*Kamati za Anna Abdallah, Lowassa zakutana

Sasa ni wazi kwamba waasi wa kundi la March 23 (M23), wamelewa kiasi cha kuomba mapambano yasimamishwe ili mazungumzo ya kuleta amani yaweze kutekelezwa. M23 wamelazimika kurudi nyuma baada ya kupigwa na Majeshi ya Umoja wa Mataifa (FIB) yanayoongozwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ). Kuna taarifa kuwa kwenye mapambano hayo, FIB waliwanasa waasi zaidi ya 1,000 na kuwanyang’anya silaha mbalimbali.