JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Siri ya Mandela

*Alisahau viatu vyake vya kijeshi Tanzania, akafungwa

*Mufti Simba, Askofu Kilaini, Ruwa’ichi watoa tamko

*Profesa Baregu, Wangwe, Safari, Kiwanuka wanena

 

Kifo cha Rais wa kwanza mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela “Madiba”, kimefichua siri nzito kuhusu harakati zake za ukombozi wa taifa hilo kutoka katika makucha ya serikali ya kibaguzi ya Wazungu.

M23 yawafika mazito

*UN waanza kutumia ndege zisizo na rubani kusaka masalia

*Zinatambua aliko mwenye bunduki, zilitumika Afghanistan

 

Baada ya Brigade Maalum ya Umoja wa Mataifa ikiongozwa na Jenerali wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuwasambaratisha waasi wa M23 nchini DRC, Brigade hiyo imeanza kutumia ndege zisizokuwa na marubani (drones) kufanya ulinzi katika mji wa Goma, hali inayozidi kuwafukizia moshi waasi hao.

Jahazi Asilia: CCM, CUF wanahofu vivuli vyao

Chama cha Jahazi Asilia kimesema mtindo unaotumiwa na vyama vya CCM na CUF kubeba wanachama kwenda na kurudi kwenye mikutano ya hadhara hauvikisaidii vyama hivyo kujitambua na kupima kisiasa kama vinakubalika au la.

M23 walia njaa

Waona giza nene mbele yao, Uganda yaonya vita inanukia
DRC yazidisha mashaka kwa Uganda, Watanzania waonya

Hatua ya Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kukataa kusaini mkataba wa amani na kundi la waasi la M23, imepeleka kilio kwa kundi hilo, na sasa wanalia njaa uhamishoni nchini Uganda.

Wastaafu  wahoji hati ya Muungano Pemba, Unguja

Wastaafu wa kada mbalimbali serikalini wameitaka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) chini ya  Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, kuonesha hati ya  Mungano wa Unguja na Pemba iwapo visiwa hivyo viliungana kisheria na mkataba kutambuliwa na Umoja wa Mataifa.

ADC: Dk. Shein anamuogopa Maalim Seif

Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC) kimesema kitendo cha Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein, kutomchukulia hatua za  kisheria Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad, kutokana na  ofisi yake kutumia vibaya fedha za umma kinyume cha sheria, kimeupaka matope utawala wake na huenda anamuogopa kiongozi huyo.