JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Hukumu yamliza bibi kizee

Hukumu ya kesi ya rufani namba 285/2012 iliyotolewa na Mahakama ya Rufaa Mkoa wa Mwanza, imemliza Bibi Kizee, Moshi Juma  Nzungu (67), kwa hofu ya kunyang’anywa nyumba anayoishi tangu miaka ya 1957 katika eneo la Pasiansi, jijini Mwanza.

Katiba haiandikiki

  • CCM, Chadema, Profesa Shivji wasema muda hautoshi
  • Jaji Mtungi aonya, mnyukano waendelea, hofu yatanda

Kuna kila dalili kuwa Katiba mpya iliyotarajiwa kuzinduliwa Aprili 26, 2014 haiandikiki kwa maana kuwa muda huo hauwezi kutosha kukamilisha mchakato wa kupata Katiba hiyo, vyanzo vimelieleza gazeti la JAMHURI.

Magufuli amvimbia Pinda

Kuna kila dalili kuwa Waziri wa Ujenzi, Dk. John Pombe Magufuli, amekataa au kushindwa kutekeleza maagizo ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kutokana na kilichoelezwa kuwa kuyatekeleza ni kuvunja sheria ya usalama barabarani na kanuni zake, hivyo yeye hayuko tayari kufanya hivyo.

TEF, MCT wampongeza Kikwete

Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Baraza la Habari Tanzania (MCT) wamempongeza Rais Jakaya Kikwete kwa hatua ya kutangaza akiwa jijini London kuwa kuanzia mwakani, Serikali itatunga Sheria ya Haki ya Kupata Habari.

Chadema ‘Kimewaka’

Chimbuko migogoro ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) unasababishwa migongano wa kupata madaraka ndani ya chama hicho, JAMHURI limebaini

Imelezwa kuwa mtafaruku uliotokea mwishoni mwa wiki na kusababisha kusimamishwa kwa Mwenyekiti wa  Mkoa wa Arusha wa Chadema  kwa muda usiojulikana ni mgongano wa kutafuta madaraka ndani ya chama hicho.

‘Majangili’ 20 hatari

  • JWTZ watisha, maofisa Maliasili 16 wakamatwa
  • Mmoja akutwa anamiliki bunduki 5 za rifle kali
  • Mbunge Mtutura ahojiwa, Nchambi naye atajwa
  • RCO aliahidiwa dola 3,000 akawaachia Waarabu

Operesheni Tokomeza inayoendeshwa chini ya usimamizi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), imewakamata watumishi kadhaa wa Serikali wanaotuhumiwa kujihusisha na ujangili. Operesheni hiyo inaongozwa na Luteni Kanali A. Sibuti.