Category: Siasa
RIPOTI MAALUMU
Majaji ‘vihiyo’ watajwa
*Yumo aliyeshindwa kuandika hukumu miaka minne
*Wengine wagonjwa, hawajawahi kusikiliza kesi
*Yumo Jaji wa Mahakama ya Rufaa asiye na shahada
*Baada ya kubanwa sasa anasoma Chuo Kikuu Huria
*Wengine walikuwa mahakimu watuhumiwa wa rushwa
Wabunge waunga mkono msimamo wa Morocco
Bunge la Tanzania linaunga mkono msimamo wa Morocco katika kupata ufumbuzi wa mgogoro kati ya taifa hilo na taifa la Sahara Magharibi. Mwaka 1975 uliibuka mgogoro wa ndani kati ya Morocco na taifa la Sahara Magharibi linalotaka kujitangazia Uhuru. Mgogoro huu uliofanya Sahara Magharibi kujenga ukuta kama wa Berlin kule Ujerumani, umekuwa na madhara makubwa ndani ya taifa la Morocco.
Malawi waigwaya kipigo JWTZ
* Taarifa za kiintelejensi za Jeshi letu zawaogopesha
* Ndege za utafiti zaondolewa upande wa Tanzania
* Makamanda wasisitiza kuendelea kuulinda mpaka
* Waingereza walipotosha mpaka
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) linaendelea kuimarisha ulinzi katika mpaka wa Tanzania na Malawi, licha ya taifa hilo dogo lililopo kusini mwa Afrika kuonyesha nia ya kutotaka kuingia katika vita, lakini pia gazeti la JAMHURI limebaini chimbuko la historia ya upotoshaji katika mpaka wa nchi hizi.
JWTZ wasogea mpakani
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Tanzania, Bernard Membe, ameionya Serikali ya Malawi kuhusu mgogoro wa mpaka, katika kile kinachoonekana kuwa Tanzania ipo tayari kuingia vitani endapo itapuuzwa. Wakati Membe akitoa msimamo huo mkali bungeni jana, kuna habari kwamba wanajeshi na vifaa vya kijeshi wameshapelekwa karibu na eneo la mgogoro ajili ya kuimarisha ulinzi.
Dk. Lwaitama: Serikali tatu hazikwepeki
Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Azavel Lwaitama (pichani), amesema suluhisho pekee la kunusuru Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni kuwa na Serikali tatu.
Dk. Lwaitama alitoa kauli hiyo katika Mazungumzo ya Asubuhi kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyoandaliwa na Baraza la Habari Tanzania na kufanyika katika Hoteli ya Court Yard jijini Dar es Salaam jana.
Serikali yaelekea kukubali hoja ya Waislamu
Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), inaelekea kulikubali ombi la kundi la waumini wa Kiislamu wanaotaka dodoso la dini liingizwe kwenye Sensa ya Watu na Makazi iliyopangwa kufanyika Agosti 26, mwaka huu.
Uamuzi huo ambao umeshawahi kupingwa na Mkurugenzi Mkuu wa NBS, Dk. Albina Chuwa, unatajwa kwamba huenda ukatangazwa hivi karibuni baada ya ngazi ya juu ya uongozi “kutafakari” na kubaini kuwa dodoso hilo haliwezi kuathiri umoja na mshikamano miongoni mwa Watanzania.
Habari mpya
- DC Simanjiro aagiza wanaoishi mabondeni wahame
- Ulega aweka mkazo mgawanyo wa rasilimali fedha za barabara Pwani
- Dk Muyungi asisitiza ujenzi wa jengo la OMR, Mtumba Dodoma
- Tanzania yashika nafasi ya nne kwa uwekezaji sekta ya madini Afrika
- NIDA yaongeza mashine, siku za usajili Mbeya
- Migogoro ya mahusiano bado ni changamoto- CRC
- Rais Samia kuifugua Rukwa kimiundombinu
- Dk. Gwajima awahimiza wananchi kuupokea na kuulinda mradi wa pamoja kwa ustawi wa jamii
- Soma Gazeti la Jamhuri Machi 10-16, 2026
- Wataalam wa fedha SADC wajadili vyanzo vya kuongeza bajeti
- UN yaipongeza Tanzania kwa juhudi za kurejesha amani, kuimarisha taasisi za kidemokrasia
- Wanawake Manyara wawatunuku tuzo maalum ya kutambua mchango wa RC Sendiga, Ras Muhaji
- Tuzo ya Korani ya kimataifa yaiva
- Dk Mwigulu : Serikali inatambua uwepo wa watumishi wachapakazi
- Serikali yasisitiza matumizi ya PPP kuchochea maendeleo ya taifa