JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Kitaifa

Serikali: Ardhi ni ya Watanzania tu

*Yawaonya wageni waliojipenyeza kuimiliki kinyemela

Serikali imeendelea kuwapiga marufuku wageni kutoka mataifa jirani na Tanzania, kujipenyeza na kumiliki ardhi kinyemela hapa nchini.

Bunduki za mbunge zanaswa kwa ujangili

*Zakutwa kwa msaidizi wake, ahukumiwa miaka miwili

*Mwenyewe atoa shutuma nzito bungeni dhidi ya polisi

Bunduki tatu za Mbunge wa Tunduru Kusini, Mtutura Mtutura, zimekamatwa kwa matukio ya ujangili katika Pori la Selous- Niassa, lililopo Tunduru -mpakani kwa Tanzania na Msumbiji.

TBS yaendelea kudhibiti bidhaa feki

Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Joseph Masikitiko, amesema shirika hilo limeteketeza nondo tani 500 zenye thamani ya Sh bilioni 8, baada ya kubaini hazina ubora unaotakiwa kwa ajili ya matumizi ya ujenzi.

Siku za Ekelege TBS zahesabika

Wakati wowote kuanzia sasa Mkurugenzi wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS) aliyesimamishwa kazi mwaka mmoja uliopita, Charles Ekelege atapandishwa kizimbani kujibu tuhuma za rushwa na matumizi mabaya ya ofisi.

RIPOTI MAALUMU

IGP Mwema ampa hifadhi ‘muuaji’ wa Barlow

*Apewa ulinzi wa polisi wenye silaha

*Anapewa huduma zote za kibinadamu

*Mbunge, Naibu Waziri wahusishwa ujangili

Kijana Mohamed Malele aliyejisalimisha kwenye vyombo vya ulinzi na usalama akijitambulisha kuwa mshirika wa mtandao uliohusika kumuua Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Liberatus Barlow, amepewa ulinzi maalumu.

Ni Bajeti ya Karne ya 22

*Asilimia 90 ya Bajeti ya Wizara zapelekwa kwenye maendeleo

*Wamarekani wamwaga mabilioni mengine kwenye MCC

*Mtwara, Lindi wapendelewa, kuunganisha umeme Sh 99,000

*Wizara yasisitiza ujenzi bomba kutoka Mtwara upo palepale

 

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, amesoma Bajeti ya wizara hiyo ya mwaka wa fedha wa 2013/2014 na kusema asilimia 90 ya fedha zinazoombwa ni kwa ajili ya maendeleo; na hivyo kuifanya kuwa ni maalumu kwa ajili ya kuiingiza Tanzania katika karne ya 22.