JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Maoni ya Mhariri

Rais chukua hatua, nchi inamalizwa

Watu wengi wameshtushwa na habari kwamba Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) imetumia Sh bilioni tisa kwa ajili ya posho kwa kikao cha wafanyakazi wa Mamlaka hiyo.

Serikali ilipe madeni mifuko ya jamii

Hivi karibuni Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Jamii (SSRA) iliwekwa ‘kitimoto’ na Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) iliyo chini ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe na makamu wake, Deo Filikunjombe wa Ludewa.

Tuwe makini kuelimisha wananchi Katiba Mpya

Tayari Bunge Maalumu la Katiba limepitisha rasimu ya Katiba inayopendekezwa.

Rasimu hiyo iko tayari kwa ajili ya kupelekwa kwa wananchi kupigiwa kura baada ya kupata akidi ya theluthi mbili iliyotakiwa kisheria kwa upande wa Tanzania Bara na Visiwani.

Wanaoiponda UDA wamekosa uzalendo

Tumetafakari kwa kina juu ya taarifa zinazolaumu “Serikali kubariki ufisadi wa UDA.” Lawama hizo hutolewa na Watanzania wachache sana wanaopinga Kampuni ya wazawa ya Simon Group kuuziwa hisa za UDA.

Hoja za msingi malalamiko hayo ni kwamba Simon Group haikufuata taratibu na sheria, na pia kwamba haikuzingatia thamani halisi ya shirika hilo. Tunachofahamu sisi kwa sasa ni kwamba uuzwaji huo uko sahihi na hakuna kinachoweza kubadilika, kwani taratibu na sheria zote zilizingatiwa kikamilifu wakati wa uuzaji wa hisa za UDA kwa Simon Group.  

Ahsante TMF, Kazi ipo kwetu

  Miongoni mwa habari zilizopamba gazeti hili leo ni taarifa ya Mfuko wa Vyombo vya Habari nchini (TMF), kutoa ruzuku ya Sh. bilioni 1.7 kwa vyombo vya habari 16.Awali ya yote tunaupongeza mfuko huo kwa namna inavyoratibu shughuli zake na…

UKAWA mwaweza kuchagua vita, amani

Kwa muda wa miaka mitatu nchi yetu imeshuhudia mnyukano wa mchakato wa kupata Katiba mpya. Mnyukano huu ulianza rasmi mwaka 2011 Rais Jakaya Kikwete alipotangaza kuandikwa kwa Katiba mpya. Tangazo la Rais Kikwete lilianzisha mchakato wa kutungwa kwa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, ambayo hatimaye imelifikisha taifa katika kupata rasimu.