JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Gerezani na vitu feki Uingereza

MIAKA ya 1990 baada ya kubahatika kununua kagari kangu mgongo wa chura, nilipitia machungu baada ya kuibiwa saiti mira. Nilijaribu kujiganga bila mafanikio, kwa sababu nilikuwa nimejikung’uta kila senti mfukoni nami niwe na gari na kuliweka barabarani kwa kujidai.

Katiba Mpya, Tanzania Mpya

Mpendwa msomaji wa makala ya Katiba Mpya, Tanzania Mpya, wiki iliyopita nilianza kuzungumzia historia ya Muungano wetu, jinsi ulivyoanza kama fikra na utashi wa viongozi waasisi wa taifa letu la Tanzania.

 

Wakati haya yanatokea sikuwapo, lakini nafurahi kwa sababu nimeisoma vizuri historia ya nchi yangu. Historia inatueleza mambo mengi, na ni vyema hata kuujua mfumo wa Muungano tulionao ulitoka wapi na matatizo yalianzia wapi? 

Leo niendelee tulipoishia wiki iliyopita ili baadaye tupate kujibu swali la je, tunayo ya kujadili kuhusu Muungano? Kama tunayo, tuyajadili katika mtindo gani?

Wabongo roho mbaya hadi Ulaya?

Kuna watu huwa wanafikiria wenzao walio ughaibuni – Ulaya, Marekani au hata Mashariki ya Kati – ni wachawi. Halafu kuna wengine walikuwa wakisema kuwa labda waliotoka Tanzania na sehemu nyingine za Afrika kwenda huko na kupata maendeleo, walibebwa au ni kubarikiwa tu.

Huu ndio uzuri, ubaya wa Naibu Waziri wa Habari

Nimefanya naye kazi kwa karibu kuanzia Mei 28 hadi Novemba 3, 2007 na kisha Septemba 30, 2009 hadi Septemba 24, 2010.

Katiba mpya itakimudu kizazi cha ‘FACEBOOK?’

Suala la maisha na siasa ni kama lile fumbo la yai na kuku. Kipi kinaanza kati ya siasa na maisha. Ni siasa ndiyo inayozaa maisha ama ni maisha ndiyo yanayozaa siasa? Kipi ni mzazi wa kingine?

KATIBA MPYA ITAKIMUDU KIZAZI CHA ‘FACEBOOK?’

“Nasema Katiba ya kweli ya Watanzania inapaswa kuandikwa katika mioyo na utashi wao, na wala si ya kuandikwa kama hii tunayoililia sasa”.