JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Ni chongo au kengeza?

Kuna msemo wa Kiswahili usemao ‘akipenda chongo huita kengeza’. Nimetoa msemo huu kwa nia njema tu ya kutaka kuangalia matukio kadhaa ya vurugu au ghasia, yanayotokea mara kwa mara hapa nchini na kusababisha baadhi ya watu wanaokuwa maeneo ya matukio kuumia, kujeruhiwa na wengine kupoteza maisha yao.

Mkurugenzi: Wananchi Bukoba tulieni

*Asema ripoti ya CAG itatoa mwelekeo*Pande zinazovutana zaandaa ‘bakora’ Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, Limbakisye Shimwela, amewaomba wakazi wa Manispaa hiyo kuwa watulivu na kusubiri majibu yatakayotolewa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG) baada ya ukaguzi…

Yah: Sasa ndiyo nawakumbuka waliokuwa viongozi wazalendo

 

Huwa naona kama naota ndoto nzito, ambazo hazina mwisho kila ninaposikia vioja vya watendaji wa Serikali yetu katika kulitendea haki Taifa hili.

Napata taabu kukubaliana kama hawa ndiyo viongozi tuliowapigia kura ama walichaguliwa na Mungu, kuja kutuhukumu tungali hai kama vile mwisho wa dunia umefika.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

‘Kutegemea kubaya kupita kote ni kutegemea mtu mwingine kwa mawazo

Katika sehemu iliyopita, Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere alisema hata angekuwa anafuata sera za kibepari, angejenga viwanda. Anasema mabepari ndiyo walioanza kujenga viwanda, na viwanda vyenyewe havikuwa na sera. Ifuatayo ni sehemu ya hotuba ya Mwalimu aliyoitoa katika kilele cha Sherehe za Mei Mosi, mwaka 1995 mkoani Mbeya.Juzi

Rais Kagame si wa kumwamini sana

Makala iliyopita ya “JWTZ nginjangija Goma hadi Kigali’, imenifumbua macho. Nimepata simu nyingi na ujumbe wa maandishi usio idadi. Wapo waliotumia lugha kali, lakini wengi walikuwa waungwana. Hiyo ndiyo raha ya mijadala. Kuna wakati tunaweza kukubaliana kwenye baadhi ya mambo, na wakati mwingine tusikubaliane kwa hoja fulani fulani. Muhimu ni kujenga moyo wa uvumilivu na staha.

Kambi ya upinzani walitoka na hoja zao

Wiki iliyopita, Mkutano wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ulikuwa na vibweka na vimbwanga vingi vyenye kuacha kinywa wazi kwa mshangao na hamaki kwa mtu yeyote makini mwenye kuujali mustakabali mwema wa nchi yake.

Hata hivyo, pamoja na vibweka na vimbwanga vilivyotokea kwenye kikao hicho, ukweli unabaki kuwa kilikuwa kikao chenye moja ya miswada muhimu yenye kipekee unaokwenda kuweka jiwe jipya la msingi kwa Tanzania tunayoihitaji kuijenga kwa miaka 50, au hata 100 ijayo.