JAMHURI MEDIA

Tunaanzia wanapoishia wengine

Category: Siasa

Ansar Sunni: Hatumtambui Sheikh Ponda

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Waislamu wa Ansar Sunni, Sheikh Salim Abdulrahim Barahiyan, amesema jumuiya hiyo haina uhusiano na Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Waislamu Tanzania, Sheikh Ponda Issa Ponda. “Mimi sijawahi kukaa na Sheikh Ponda katika kikao hata kimoja. Tuna misikiti karibu 20 Tanga, hajawahi kuingia hata msikiti mmoja,” amesema Sheikh Barahiyan.

Barua ya wazi kwa Waziri Mwakyembe

Mheshimiwa Waziri Dk. Harrison Mwakyembe, tunayo heshima kuchukua nafasi hii kukujulisha kuwa matrekta haya unayoyaona yamekwishalima sana na sasa hayawezi kazi hiyo tena. Ukiyafukuza mjini ni wazi hayatakwenda kulima, maana mengi hayana uwezo tena wa kufanya kazi hiyo.

MAANDIKO YA MWALIMU NYERERE

Tujisahihishe: Mwalimu Nyerere

 

UMOJA wa kundi lolote ni sawa sawa na umoja wa viungo mbalimbali vya mwili au mtambo. Viungo vya mwili havina budi vitii kanuni zinazoviwezesha kufanya kazi yake sawa sawa. Lakini haviwezi kutii kanuni hizo kama haviko katika hali ya afya njema. Mara kiungo kimoja kinapokuwa hakina afya safi, huanza kuvunja kanuni za kazi na mwili mzima hupata taabu.

KAULI ZA WASOMAJI

Wanahabari tembeleeni pia vijijini

Waandishi wa habari jaribuni kutembelea pia na maeneo ya vijijini kwa sababu huko kuna matukio mengi ya kutisha na kusikitisha, lakini vyombo vya habari vimekuwa havielekezi nguvu kubwa vijijini kama vinavyofanya maeneo ya mijini.

Obe Mlemi, Mugumu – Serengeti

0768 235 817

JAMHURI YA WAUNGWANA

Wakati mwingine Wakristo
wanaanzisha chokochoko

Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) imewasilisha mapendekezo, ikitaka kubadilishwa kwa siku ya kupiga kura ya maoni kutoka siku ya ibada – Jumapili. Mapendekezo ya CCT yamewasilishwa kwenye Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba, Sheria na Utawala. Mwakilishi wa CCT, Mchungaji Lazaro Rohho, anasema mabadiliko hayo yanatakiwa kuwekwa kwenye muswada wa kura ya maoni unaotarajiwa kuwasilishwa katika kikao kijacho cha Bunge.

Serikali imejipanga kuiangusha CCM

Kama tujuavyo, Serikali ya leo ya Tanzania ni ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Ni sawa na kusema kwamba Serikali ni mtoto wa CCM.