Category: Siasa
NUKUU ZA WIKI
Nyerere: Elimu inayotolewa ituwezeshe kujiamini
“Elimu inayotolewa lazima ijenge akili ya kuuliza, uwezo wa kujifunza na uwezo wa kujiamini kama raia huru na sawa katika jamii.”
Maneno haya ni ya Mwasisi na Baba wa Taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
Udini sasa nongwa (2)
Ningependa nioneshe pia kuwa wapo wasomi wasiojiamini kabisa ingawa wana shahada za vyuo viikuu. Kama si upotoshaji wa kukusudia, basi hawana elimu (not liberated mentally), ni wajinga ingawa wamesoma (have been to school but not educated).
Tatizo la Kusini wanaamini wanaonewa
Ninatoka kusini mwa Tanzania mkoani Mtwara. Matukio yaliyotokea humo hasa kuanzia Desemba 2012 hapana shaka yamewashtua na kuwashangaza watu wengi.
Tuache kufyatua maneno
Habari yenye kichwa cha maneno, “Waziri achafua hewa mazishi ya Padri Z’bar” iliyochapishwa Februari 21, 2013, ilinikumbusha agizo la Rais mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa (pichani chini), aliyetuasa akisema “Kama hujafanya utafiti, huna haki ya kuzungumza”.
NUKUU ZA WIKI
Nyerere: Tushirikishe watu katika maendeleo
“Kama maendeleo ya kweli ni kuchukua mahali, watu wanapaswa kushirikishwa.”
Hii ni sehemu ya maneno ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere katika kitabu chake cha Uhuru na Maendeleo, 1973.
Tunataka Katiba halisi ya kudumu
Kama tujuavyo, hivi sasa Taifa letu liko katika mchakato wa kutafuta Katiba mpya ya nchi.
Katiba tunayotafuta sasa itakuwa nafasi ya katiba ya kudumu iliyoanza kutumika mwaka 1977. Katiba ya nchi tunayotaka kuachana nayo imedumu kwa mbinde kwa sababu ina kasoro nyingi zilizoanza kupigiwa kelele tangu mwaka 1992, wakati Tanzania ilipoingia kwenye mfumo wa vyama vingi.